IFM yang’ara mashindano ya TIOB

Na Mwandishi Wetu

CHUO cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kimeendelea kuonyesha ubora wake baada ya kushinda mashindano ya The Tanzania Institute of Bankers (TIOB) Scholar Banking Challenge kwa mfululizo wa miaka miwili, ambapo mwaka huu pia kimeongoza miongoni mwa vyuo vikuu zaidi ya 50 vilivyoshiriki.

Hayo yalisemwa juzi na Grace Kazoba, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko cha IFM, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya chuo hicho katika mashindano hayo.

Kazoba alibainisha kuwa kati ya wanafunzi 3,500 waliojitokeza kushindana, IFM imeonyesha ushindi mkubwa kwa kuwa na wanafunzi tisa bora wa kwanza kutoka chuo hicho.

“Wanafunzi wetu walishiriki kwa ushindani mkubwa na kufanya vizuri hadi kutwaa nafasi za juu zaidi,” alisema.

Aidha, alifafanua kuwa mwaka jana, wanafunzi wa IFM wa Shahada ya Sayansi katika Uchumi na Fedha (BEF) walishiriki katika mashindano ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) 2024, ambapo walionyesha jinsi ya kutengeneza faida kubwa kupitia ushiriki wa soko la hisa.

“Mwanafunzi anaamka asubuhi akifuatilia kampuni zinazofanya vizuri, na kwa kufanya hivyo kwa muda mrefu, wengi wetu walifanikiwa,” aliongeza Kazoba.

Alisema pia kuwa katika orodha ya sifa bora 30, wanafunzi wengi walitoka IFM, ambapo walionyesha uhalisia wa hali halisi wa soko la hisa na kupata tuzo kwa juhudi zao.

Ushindi huu unaonesha IFM kuendelea kuwa chuo kinachotoa elimu bora katika fani za fedha na uchumi, na kuhimiza wanafunzi wake kushindana kitaalamu na kufanikisha malengo yao katika sekta ya fedha nchini.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...