Aliyerejeshwa awabwaga wapinzani wake Kunduchi, aongoza kura za maoni

Na Mwandishi Wetu

Mgombea wa udiwani Kata ya Kunduchi, jijini Dar es Salaam anayetetea nafasi yake Michael Urio ameibuka kinara katika kura za maoni kwa kuwabwaga wagombea wengine wa wanne kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Urio ambaye ni Naibu Meya wa Manispaa ya Kinondoni, awali jina lake halikurudi wakati wa uteuzi lakini baadaye alirejeshwa.

Kwa mujibu wa matokeo ya kura za maoni yaliyotangazwa na msimamizi wa Kata hiyo leo Agosti 4, 2025 Urio ameongoza kwa kupata kura 257, anayefuatia Joyce Haule kura 250, Emmanuel Mkuchu hura 240, Hashemi Komba kura 30 na Happyness Justin alipata kura 12.

Urio ni miongoni mwa wagombea waliorejeshwa baada ya Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoa maelekezo kwa makatibu wa mikoa wa chama hicho kuwarejesha wagombea wote waliopitishwa na Kamati Siasa za mikoa ili wakapigiwe kura za maoni.

Kutokana na ushindi huo amejiweka katika nafasi ya kupitishwa kuwa mgombea wa udiwani katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29,2025.

spot_img

Latest articles

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

Mradi wa upanuzi Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kinyerezi I Extension umekamilika

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi...

More like this

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...