Aliyerejeshwa awabwaga wapinzani wake Kunduchi, aongoza kura za maoni

Na Mwandishi Wetu

Mgombea wa udiwani Kata ya Kunduchi, jijini Dar es Salaam anayetetea nafasi yake Michael Urio ameibuka kinara katika kura za maoni kwa kuwabwaga wagombea wengine wa wanne kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Urio ambaye ni Naibu Meya wa Manispaa ya Kinondoni, awali jina lake halikurudi wakati wa uteuzi lakini baadaye alirejeshwa.

Kwa mujibu wa matokeo ya kura za maoni yaliyotangazwa na msimamizi wa Kata hiyo leo Agosti 4, 2025 Urio ameongoza kwa kupata kura 257, anayefuatia Joyce Haule kura 250, Emmanuel Mkuchu hura 240, Hashemi Komba kura 30 na Happyness Justin alipata kura 12.

Urio ni miongoni mwa wagombea waliorejeshwa baada ya Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoa maelekezo kwa makatibu wa mikoa wa chama hicho kuwarejesha wagombea wote waliopitishwa na Kamati Siasa za mikoa ili wakapigiwe kura za maoni.

Kutokana na ushindi huo amejiweka katika nafasi ya kupitishwa kuwa mgombea wa udiwani katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29,2025.

spot_img

Latest articles

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

More like this

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...