Aliyerejeshwa awabwaga wapinzani wake Kunduchi, aongoza kura za maoni

Na Mwandishi Wetu

Mgombea wa udiwani Kata ya Kunduchi, jijini Dar es Salaam anayetetea nafasi yake Michael Urio ameibuka kinara katika kura za maoni kwa kuwabwaga wagombea wengine wa wanne kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Urio ambaye ni Naibu Meya wa Manispaa ya Kinondoni, awali jina lake halikurudi wakati wa uteuzi lakini baadaye alirejeshwa.

Kwa mujibu wa matokeo ya kura za maoni yaliyotangazwa na msimamizi wa Kata hiyo leo Agosti 4, 2025 Urio ameongoza kwa kupata kura 257, anayefuatia Joyce Haule kura 250, Emmanuel Mkuchu hura 240, Hashemi Komba kura 30 na Happyness Justin alipata kura 12.

Urio ni miongoni mwa wagombea waliorejeshwa baada ya Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoa maelekezo kwa makatibu wa mikoa wa chama hicho kuwarejesha wagombea wote waliopitishwa na Kamati Siasa za mikoa ili wakapigiwe kura za maoni.

Kutokana na ushindi huo amejiweka katika nafasi ya kupitishwa kuwa mgombea wa udiwani katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29,2025.

spot_img

Latest articles

Watanzania Watakiwa Kujitokeza Kuomba Nafasi 1,150 za Udereva Qatar

Na Mwandishi Wetu WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa ya ajira iliyotangazwa na...

CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini...

MAB yateta na wadhibiti Mutukula OSBP

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa TMDA (MAB), Eric Shitindi...

More like this

Watanzania Watakiwa Kujitokeza Kuomba Nafasi 1,150 za Udereva Qatar

Na Mwandishi Wetu WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa ya ajira iliyotangazwa na...

CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini...