Nandy ahamasika kutangaza Nembo ya Made in Tanzania Kimataifa

Na Tatu Mohamed

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga (Nandy), amesema elimu aliyoipata katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) imefungua macho yake kuhusu umuhimu wa kutumia nembo ya Made in Tanzania katika shughuli zake za biashara na ubunifu.

Nandy, ambaye pia ni mjasiriamali anayejihusisha na biashara ya urembo, amesema awali alikuwa anaamini bidhaa bora lazima zitoke nje ya nchi, lakini sasa amehamasika kuzalisha ndani ya nchi baada ya kufahamu nguvu ya nembo ya Made in Tanzania.

“Nimepata elimu kubwa sana, kumbe naweza kuzalisha bidhaa zangu hapa hapa nchini na bado zikawa na hadhi ya kimataifa kwa kutumia nembo ya Made in Tanzania. Hili limenifungua macho na kunipa motisha mpya,” amesema Nandy wakati alipotembelea Banda la Made in Tanzania.

Amesema anatambua nafasi yake kama msanii mwenye ushawishi mkubwa, hivyo atatumia jukwaa hilo kuelimisha na kuhamasisha vijana wengine kuhusu uzalendo wa kutumia bidhaa za ndani zenye ubora.

Nembo ya Made in Tanzania, inayosimamiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), inalenga kukuza utambulisho wa bidhaa za Kitanzania kwenye masoko ya ndani na ya kimataifa.

Kwa upande wake, Nandy ameahidi kuendelea kushiriki katika mafunzo mbalimbali ili kuwa balozi bora wa kuitangaza nembo hiyo duniani kupitia kazi zake za sanaa na bidhaa zake za kibiashara.

spot_img

Latest articles

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

TMA yatangaza msimu wa Kipupwe Juni hadi Agosti

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa na msimu...

More like this

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...