IST Festival yatumika kunadi mitaji nafuu kwa vijana

Na Mwandishi Wetu

TAMASHA la IST Festival lililofanyika jana Februari 14, 2026 kwenye viwanja vya Fukwe za Coco jijini Dar es Salaam limekuwa jukwaa mahsusi la kuwafikia vijana na wanawake kwa kuwapatia fursa za uwezeshaji kiuchumi na elimu ya afya.

Kupitia tamasha hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Jiji la Dar es Salaam, wadau mbalimbali walitumia fursa hiyo kutoa elimu na kutangaza huduma zao.

Miongoni mwa wadhamini wakuu wa tamasha hilo ni Benki ya CRDB kupitia CRDB Bank Foundation, ambao walitumia mkusanyiko huo mkubwa wa vijana kunadi Programu za Go Green na Imbeju zinazolenga kutoa mitaji nafuu kwa vijana wenye miradi bunifu inayohusiana na kilimo, nishati na uhifadhi wa mazingira.

Akizungumza katika tamasha hilo, Meneja Mwezeshaji kutoka CRDB Bank Foundation, Shamiri Kamtu, amesema dirisha la maombi ya mikopo kupitia Programu ya Imbeju na Go Green limefunguliwa rasmi, na kwamba vijana kote nchini wanapaswa kuchangamkia fursa hiyo kabla ya Machi 11, ambayo ni mwisho wa kutuma maombi.

Amesema programu hizo zimeanzishwa kimkakati kuwainua vijana wanaojihusisha na mnyororo mzima wa thamani wa kilimo, huku zikihamasisha matumizi ya teknolojia na nishati safi rafiki kwa mazingira.

Katika hatua nyingine, kampuni tanzu ya CRDB Insurance Company ilitoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa bima na kutoa huduma za bima papo kwa papo kwa washiriki wa tamasha hilo.

Akizungumza kwa niaba ya kampuni hiyo, Omary Melele amesema wameimarisha mifumo ya ulipaji madai ili kuhakikisha wateja wanalipwa kwa wakati na kwa urahisi, akiwahamasisha Watanzania kujiwekea kinga kupitia huduma za bima.

Tamasha la IST Festival limeendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwaunganisha vijana, kuwafungulia fursa za kiuchumi na kuwapatia elimu ya afya kwa maendeleo endelevu ya taifa.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...