Dk.Jingu awashauri vijana kujiandaa kwa uzee

Na Mwandishi Wetu

‎Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. John Jingu, ametoa wito mahsusi kwa vijana na jamii kwa ujumla kujiandaa kwa maisha ya uzee kwa kutumia vizuri rasilimali walizonazo. 

“Ni muhimu vijana wawe na mtazamo wa muda mrefu kwa kuwekeza katika familia, mahusiano mema na miradi ya kiuchumi ambayo itawasaidia wanapoingia uzeeni. Ujana ni hatua ya maandalizi ya uzee, tusikimbie wajibu huu,”

Dk. Jingu ameyasema hayo Julai 03, 2025 alipotembelea Makazi ya Wazee cha Bukumbi yaliyopo mkoani Mwanza kwa lengo la kuwajulia hali wazee wanaoishi katika Makazi hayo pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili.

Aidha ameitaka jamii kushiriki kikamilifu katika kuwatunza wazee wao, kuwaheshimu, kuwaangalia na kulinda dhidi ya vitendo vya kikatili.

‎Katika ziara hiyo, Dk. Jingu amehimiza pia wazee kushiriki katika Uchaguzi Mkuu pamoja na fursa mbalimbali za kiuchumi, ikiwemo zile zinazotolewa kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA). 

‎Katika hatua nyingine,ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mahabusu ya watoto jijini Mwanza ambapo ameeleza kuridhishwa na hatua iliyofikiwa kwani mradi huo umefikia asilimia 90 ya utekelezaji. Ujenzi wa mahabusu hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya Tume Maalum iliyoundwa ili kuboresha Taasisi za haki jinai nchini hususan zinazohusiana na watoto.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...