Esther Bulaya: Nilikuwa Chadema kwa mkopo nimerejea, CCM ni kama  Barcelona 

Na Mwandishi Wetu

Aliyekuwa Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Esther Bulaya  amesema  alikuwa Chadema kwa mkopo sasa amerejea  Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ni sawa Barcelona  au Real Madrid na wanakwenda kutengeneza kikosi cha kushinda ‘Champions League’.

Bulaya   ambaye  amerejea  CCM na kuchukua fomu ya kugombea Ubunge, Jimbo la Bunda Mjini mkoani Mara kupitia CCM, amejinasibu  mbele ya waandishi wa habari kuwa  chama alichokuwepo ni kama timu iliyoshuka daraja, hivyo amerudi kutoka kwenye mkopo.

“Unapozngumzia Chama Cha Mapinduzi  ndio Barcelona ya Tanzania, Chama Cha Mapinduzi  kimerudisha usajili kwa wachezaji wake wa Barcelona ambao waliwatuma kwa mkopo kwenye timu ya Leicester City  ambayo imeshuka daraja,” amesema Bulaya.

Ameeleza kuwa alianza  harakati  ndani ya CCM tangu akiwa  vyuoni, hivyo  ana furaha kurejea katika chama kilichomlea.

Bulaya ni miongoni mwa wabunge 19 wa Viti Maalumu wa CHADEMA ambao chama hicho kilitangaza kuwavua uanachama, lakini walisalia bungeni hadi kuhitimishwa kwa Bunge la 12 kwa amri ya mahakama.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...