Esther Bulaya: Nilikuwa Chadema kwa mkopo nimerejea, CCM ni kama  Barcelona 

Na Mwandishi Wetu

Aliyekuwa Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Esther Bulaya  amesema  alikuwa Chadema kwa mkopo sasa amerejea  Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ni sawa Barcelona  au Real Madrid na wanakwenda kutengeneza kikosi cha kushinda ‘Champions League’.

Bulaya   ambaye  amerejea  CCM na kuchukua fomu ya kugombea Ubunge, Jimbo la Bunda Mjini mkoani Mara kupitia CCM, amejinasibu  mbele ya waandishi wa habari kuwa  chama alichokuwepo ni kama timu iliyoshuka daraja, hivyo amerudi kutoka kwenye mkopo.

“Unapozngumzia Chama Cha Mapinduzi  ndio Barcelona ya Tanzania, Chama Cha Mapinduzi  kimerudisha usajili kwa wachezaji wake wa Barcelona ambao waliwatuma kwa mkopo kwenye timu ya Leicester City  ambayo imeshuka daraja,” amesema Bulaya.

Ameeleza kuwa alianza  harakati  ndani ya CCM tangu akiwa  vyuoni, hivyo  ana furaha kurejea katika chama kilichomlea.

Bulaya ni miongoni mwa wabunge 19 wa Viti Maalumu wa CHADEMA ambao chama hicho kilitangaza kuwavua uanachama, lakini walisalia bungeni hadi kuhitimishwa kwa Bunge la 12 kwa amri ya mahakama.

spot_img

Latest articles

TRA yawaalika wananchi Sabasaba kupata elimu ya Kodi na huduma za TIN

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imewaita wananchi kutembea banda lao lililopo katika...

2020 Vunjo primaries leader to challenge Dr. Kimei again

Enock Koola (35), a staunch member of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party...

Makamu wa Rais atoa wito uboreshaji mfumo wa fedha

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya...

Kihongosi aahidi kutekeleza alichoagizwa na Rais Samia  Arusha

Na Mwandishi Wetu  Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha,  Kenani Kihongosi amesema  atafanya kazi aliyotumwa na Rais...

More like this

TRA yawaalika wananchi Sabasaba kupata elimu ya Kodi na huduma za TIN

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imewaita wananchi kutembea banda lao lililopo katika...

2020 Vunjo primaries leader to challenge Dr. Kimei again

Enock Koola (35), a staunch member of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party...

Makamu wa Rais atoa wito uboreshaji mfumo wa fedha

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya...