Kaboyoka ajiunga rasmi na ACT Wazalendo

Na Tatu Mohamed

MBUNGE wa Viti Maalum wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha 2020 hadi 2025, Nagy Livingstone Kaboyoka, amejiunga rasmi na Chama cha ACT Wazalendo.

Hafla ya mapokezi imefanyika leo katika Ukumbi wa Hakainde Hichilema uliopo Makao Makuu ya ACT Wazalendo, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Kaboyoka amepokelewa na Kiongozi wa Chama hicho, Ndugu Dorothy Semu, pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wa Ngome ya Wanawake wa ACT Wazalendo.

Kaboyoka ni mzoefu katika siasa za Tanzania na amewahi kushika nafasi mbalimbali zenye ushawishi.

Alikuwa Mbunge wa kuchaguliwa wa Jimbo la Same Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kati ya mwaka 2015 hadi 2020, ambapo alimshinda aliyekuwa Mbunge wa CCM, Anne Kilango Malecela.

Aidha, amehudumu kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa miaka 10 mfululizo, kuanzia mwaka 2015 hadi 2025.

Ujio wa Kaboyoka ndani ya ACT Wazalendo unaelezwa kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha nguvu ya chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025, hasa katika harakati za kujenga upinzani imara na chenye dira ya uwajibikaji wa kweli kwa wananchi.

spot_img

Latest articles

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

More like this

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...