Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia (Must), mwaka wa kwanza, Emilia Joseph (21) kwa tuhuma za mauaji ya mwenzake wakiwa kwenye ‘Club’ ya Mbeya Pazuri jijini humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amedai kuwa mtuhumiwa alifanya mauaji ya mwenzake wa mwaka wa tatu Gerald Philber Said (22), baada ya kumchoma na kitu chenye ncha kali tumboni.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Jumanne Juni 17,2025,  imesema tukio hilo lilitokea Juni 14,2025 saa 11.00 alfajiri wakiwa wamelewa pombe kupita kiasi.

Amedai kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha mauaji hayo ni baada ya kuibuka ugomvi baina ya marehemu na mtuhumiwa uliotokana na matumizi ya ulevi wa pombe kupindukia.

” Baada ya kuibuka ugomvi mabaunsa walimtoa mtuhumiwa nje ambaye alienda kwenye eneo alikoegesha gari , ambapo marehemu alimfuata kwa lengo la kuendeleza ugomvi ndipo alipomchoma na kitu chenye ncha kali tumboni ,”amesema.

Amesema baada ya marehemu kubainika kudhurika ndipo wasamaria wema walimbeba na kumuwahisha katika Hospitali ya Rufaa Kanda kwa matibabu zaidi.

“Wakati madaktari wakiendelea kumpatia matibabu ilipofika saa 7.00 mchana alifariki dunia,”amesema.

Kufuatia tukio hilo Kamanda Kuzaga ameonya wanafunzi wa vyuo vikuu kuachana na matumizi ya pombe kupitia kiasi na badala yake kuzingatia masomo na kutimiza ndoto zao.

spot_img

Latest articles

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

More like this

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...