Rais Samia asisitiza maadili kwa Jeshi la Polisi 

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan amewaasa wahitimu wa kozi ya maafisa na wakaguzi wasaidizi wa Jeshi la Polisi kuwa mabalozi wa maadili na kusaidia kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea rushwa ndani ya Jeshi hilo.

Amesema hayo leo June 09,2025 Jijini Dar es Salaam wakati akishiriki sherehe ya kufunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi wa Jeshi la Polisi.

“Muwe sehemu ya kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea rushwa. Haya ndiyo maradhi makubwa yaliyokuwa ndani ya Jeshi letu. Sitaki kusema yameisha, yapo, yanaendelea. Nikirushiwa clip (inayoonesha vitendo vya rushwa), namrushia IGP, na anachukua hatua mara moja,” amesema.

Rais Samia ameliagiza jeshi hilo kuhakikisha linaimarisha maadili kwa videndo kwa maafisa na askari wake ili melinda heshima ya taasisi hiyo na kuzidi kujenga imani ya wananchi kwa combo via dola.

Amesema  mafanikio ya  Jeshi la Polishi katika kulinda  raia na mali zao hayawezi kupatikana endapo maadili kudorora miongoni mwa watendaji wake.

Kuhusu usalama barabarani amelitaka jeshi hilo kuimarisha mikakati ya kuthibiti ajali za barabarani, akisema licha ya kushuka  kwa jumla ya idadi ya ajali na vifo katika mwaka  mmoja uliopita, bado takwimu za vifo ni kubwa.

Aidha amelitaka kuongeza ubunifu na matumizi ya teknolojia kabila kudhibiti ajali hizo.

spot_img

Latest articles

Sababu za kiusalama zazuia Lissu kufikishwa mahakamani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Magereza limeshindwa kumfikisha mahakamani Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na...

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

More like this

Sababu za kiusalama zazuia Lissu kufikishwa mahakamani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Magereza limeshindwa kumfikisha mahakamani Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na...

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...