Rais Samia asisitiza maadili kwa Jeshi la Polisi 

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan amewaasa wahitimu wa kozi ya maafisa na wakaguzi wasaidizi wa Jeshi la Polisi kuwa mabalozi wa maadili na kusaidia kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea rushwa ndani ya Jeshi hilo.

Amesema hayo leo June 09,2025 Jijini Dar es Salaam wakati akishiriki sherehe ya kufunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi wa Jeshi la Polisi.

“Muwe sehemu ya kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea rushwa. Haya ndiyo maradhi makubwa yaliyokuwa ndani ya Jeshi letu. Sitaki kusema yameisha, yapo, yanaendelea. Nikirushiwa clip (inayoonesha vitendo vya rushwa), namrushia IGP, na anachukua hatua mara moja,” amesema.

Rais Samia ameliagiza jeshi hilo kuhakikisha linaimarisha maadili kwa videndo kwa maafisa na askari wake ili melinda heshima ya taasisi hiyo na kuzidi kujenga imani ya wananchi kwa combo via dola.

Amesema  mafanikio ya  Jeshi la Polishi katika kulinda  raia na mali zao hayawezi kupatikana endapo maadili kudorora miongoni mwa watendaji wake.

Kuhusu usalama barabarani amelitaka jeshi hilo kuimarisha mikakati ya kuthibiti ajali za barabarani, akisema licha ya kushuka  kwa jumla ya idadi ya ajali na vifo katika mwaka  mmoja uliopita, bado takwimu za vifo ni kubwa.

Aidha amelitaka kuongeza ubunifu na matumizi ya teknolojia kabila kudhibiti ajali hizo.

spot_img

Latest articles

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

More like this

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...