Rais Samia asisitiza maadili kwa Jeshi la Polisi 

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan amewaasa wahitimu wa kozi ya maafisa na wakaguzi wasaidizi wa Jeshi la Polisi kuwa mabalozi wa maadili na kusaidia kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea rushwa ndani ya Jeshi hilo.

Amesema hayo leo June 09,2025 Jijini Dar es Salaam wakati akishiriki sherehe ya kufunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi wa Jeshi la Polisi.

“Muwe sehemu ya kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea rushwa. Haya ndiyo maradhi makubwa yaliyokuwa ndani ya Jeshi letu. Sitaki kusema yameisha, yapo, yanaendelea. Nikirushiwa clip (inayoonesha vitendo vya rushwa), namrushia IGP, na anachukua hatua mara moja,” amesema.

Rais Samia ameliagiza jeshi hilo kuhakikisha linaimarisha maadili kwa videndo kwa maafisa na askari wake ili melinda heshima ya taasisi hiyo na kuzidi kujenga imani ya wananchi kwa combo via dola.

Amesema  mafanikio ya  Jeshi la Polishi katika kulinda  raia na mali zao hayawezi kupatikana endapo maadili kudorora miongoni mwa watendaji wake.

Kuhusu usalama barabarani amelitaka jeshi hilo kuimarisha mikakati ya kuthibiti ajali za barabarani, akisema licha ya kushuka  kwa jumla ya idadi ya ajali na vifo katika mwaka  mmoja uliopita, bado takwimu za vifo ni kubwa.

Aidha amelitaka kuongeza ubunifu na matumizi ya teknolojia kabila kudhibiti ajali hizo.

spot_img

Latest articles

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...

Rostam aanika maono yake umiliki mpya ya NMG

Na Mwandishi Wetu MFANYABIASHARA na mwekezaji wa Tanzania, Rostam Azizi, ametangaza uwekezaji mkubwa wa kimkakati...

More like this

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...