Makanisa sita ya Gwajima yafungiwa  Mbeya

Na Mwandishi wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeyafungia matawi sita ya Kanisa la Ufufuo na Uzima yaliyokuwa yakiendelea  na huduma katika maeneo tofauti mkoani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 6,2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga  amesema kufungiwa kwa matawi hayo ni kunatokana na tamko la Serikali lililotolewa Juni 2, 2025 kupitia Msajili wa Jumuiya za kiraia nchini la kufunga makanisa ya Ufufuo na Uzima kutoendelea kutoa huduma katika matawi yake.

Kamanda Kuzaga amesema kuwa matawi ya Kanisa la Ufufuo na Uzima yaliyofungiwa ni pamoja na la lililopo ZZK katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi Mbeya vijijini pamoja na lililopo mtaa wa Mnadani katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa wilayani Mbarali.

Mengine yaliyofungiwa ni yaliyopo katika Halmashauri za Wilaya za Chunya, Rungwe, Kyela pamoja na Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Ameeleza kuwa bado ufuatiliaji unafanyika kuhakikisha wanayafungia wote na kuwataka viongozi na waumini  kuacha kuendesha  shughuli za vidimi katika makanisa hayo.

spot_img

Latest articles

Dkt. Biteko: Dunia inaiangalia Tanzania na Afrika Mashariki kuwa Kitovu cha Utalii

📌 Atoa maagizo matatu kwa Wizara ya Maliasili 📌 Rais Samia aiweka Tanzania kwenye...

Gugu asisitiza umuhimu wa ushirikiano Kikanda kukabiliana na uhalifu

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  Ally Gugu, amesisitiza...

Spika Tulia: Serikali Itaendelea Kupambana na Changamoto ya Mikopo kwa Wanafunz

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia...

Serikali yaja na mkakati kukabiliana na migogoro ya ardhi Morogoro

Na Mwandishi Wetu Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Geophrey  Pinda amesema...

More like this

Dkt. Biteko: Dunia inaiangalia Tanzania na Afrika Mashariki kuwa Kitovu cha Utalii

📌 Atoa maagizo matatu kwa Wizara ya Maliasili 📌 Rais Samia aiweka Tanzania kwenye...

Gugu asisitiza umuhimu wa ushirikiano Kikanda kukabiliana na uhalifu

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  Ally Gugu, amesisitiza...

Spika Tulia: Serikali Itaendelea Kupambana na Changamoto ya Mikopo kwa Wanafunz

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia...