Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

TRA yakana kuhusika na kufungwa kwa baa ya THE CASK

Na Mwandishi Wetu, Media Barains

Mamla ya Mapato Tanzania (TRA) imeeleza kuwa haihusiki na kufungwa kwa baa ya The Cask ya jijini Mwanza.

Taarifa iliyotolewa leo Agosti 17, na Idara ya Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano imewataka wahusika kuwasiliana na mamlaka husika kuhusu jambo hilo.

“Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuujulisha umma kuwa, haijahusika kwa namna yoyote na ufungaji wa Bar ya THE CASK iliyopo jijini Mwanza.

“Tunaomba wahusika na umma wawasiliane na Mamlaka husika juu ya jambo hilo,” imeeleza taarifa hiyo ya TRA.

Agosti 16, mwaka huu taarifa kutoka jijini Mwanza zilidai kuwa Serikali wilayani Ilemela iliifunga baa hiyo kwa tuhuma za ukwepaji kodi kwa kipindi cha miaka miwili.

“Serikali wilayani Ilemela mkoani Mwanza imeifunga baa maarufu ya The Cask Bar & Grill ya jijini Mwanza kwa tuhuma za ukwepaji kodi kwa kipindi cha miaka miwili.

“Kwa mjibu wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Kiomono Kibamba amesema, uongozi wa baa hiyo umekwapa kodi ya Serikali na kuendesha biashara zaidi ya moja eneo hilo hilo,” ilieleza taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...