Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

TRA yakana kuhusika na kufungwa kwa baa ya THE CASK

Na Mwandishi Wetu, Media Barains

Mamla ya Mapato Tanzania (TRA) imeeleza kuwa haihusiki na kufungwa kwa baa ya The Cask ya jijini Mwanza.

Taarifa iliyotolewa leo Agosti 17, na Idara ya Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano imewataka wahusika kuwasiliana na mamlaka husika kuhusu jambo hilo.

“Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuujulisha umma kuwa, haijahusika kwa namna yoyote na ufungaji wa Bar ya THE CASK iliyopo jijini Mwanza.

“Tunaomba wahusika na umma wawasiliane na Mamlaka husika juu ya jambo hilo,” imeeleza taarifa hiyo ya TRA.

Agosti 16, mwaka huu taarifa kutoka jijini Mwanza zilidai kuwa Serikali wilayani Ilemela iliifunga baa hiyo kwa tuhuma za ukwepaji kodi kwa kipindi cha miaka miwili.

“Serikali wilayani Ilemela mkoani Mwanza imeifunga baa maarufu ya The Cask Bar & Grill ya jijini Mwanza kwa tuhuma za ukwepaji kodi kwa kipindi cha miaka miwili.

“Kwa mjibu wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Kiomono Kibamba amesema, uongozi wa baa hiyo umekwapa kodi ya Serikali na kuendesha biashara zaidi ya moja eneo hilo hilo,” ilieleza taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...