Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Madaktari wafanikiwa kukiongezea damu kijusi ndani ya tumbo la mama

Nairobi, Kenya

Madaktari katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta nchini Kenya wamefanikiwa kutia damu kwa kijusi akiwa bado kwenye mfuko wa uzazi wa mama huyo.

Utaratibu huo wa umakini zaidi, unaojulikana kama Uhamisho wa Ndani wa Kijusi ni hatua muhimu katika matibabu ya kijusi na utaalamu wa tiba ya ndani ya mwili wa mama.

Timu ya madaktari bingwa wanne walifanya utaratibu huo wa kimatibabu ambapo chembe nyekundu za damu kutoka kwa wafadhili hudungwa ndani ya kijusi.

Uhamisho wa ndani ya mfuko wa uzazi unaweza kupendekezwa wakati kijusi kina upungufu wa damu au Anemia (hali inayopunguza seli za damu).

Madaktari hao ni pamoja na Rosa Chemwey, Flavia Ogutu, Ikol Adung’o na Kunjira Murayi, Mtaalamu wa tiba ya miale.

Walisaidiwa na Benson Nyankuru na Redempata Mumo ambao ni wauguzi, na Tony Wainaina, Afisa wa Kliniki ya Afya ya Uzazi.

Kwa kutumia kipimo cha ultrasound ili kubainisha nafasi ya kijusi na na kondo la nyuma la uzazi, daktari wa upasuaji huingiza sindano kwenye fumbatio la mama na kisha kwenye mshipa wa kitovu cha kijusi.

spot_img

Latest articles

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

More like this

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...