Simba yatua Dar na kauli ya kibabe

Na Mwandishi Wetu

Kikosi cha Simba kimewasili Dar es Salaam kikitokea Zanzibar kwenye mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi RS Berkane ambapo mashabiki wamejitokeza Bandarini kuipokea timu yao, huku Msemaji wa klabu hiyo, Ahmed Ally akisema kwa hatua waliyofikia wanajihesabu kama mabingwa wa Afrika

Amesema wameumia kukosa ubingwa wa michuano hiyo lakini hawana deni na wachezaji wao wala benchi la ufundi kwa sababu wametimiza majukumu yao na wamevuka malengo, hivyo wanajihesabu kama mabingwa wa Afrika.

“Matokeo ya kufungwa mpira wa miguu huwa ni matokeo ya kuumiza, kinachouma zaidi kombe lilikuwa uwanjani, kombe jipya limeondoka tumelikosa sisi Simba, tuna maumivu makali mno, lakini katika mioyo yetu sisi Wanasimba tunajihesabu kama ni mabingwa wa Afrika,” amesema Ahmed.

Keshokutwa kikosi hicho kitashuka dimbani katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Singida BS kwenye Uwanja wa KMC.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...