Rais Mwinyi: Tutamuenzi Charles Hilary kwa utendaji wake uliotukuka

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewaongoza Viongozi mbalimbali na mamia ya Wananchi katika maziko ya Marehemu Charles Martin Hilary, aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu.

Mapema, Rais Dkt. Mwinyi aliwaongoza Viongozi na Wananchi katika Ibada ya kuuaga mwili wa marehemu, iliyofanyika katika Viwanja vya Mapinduzi Square, Michenzani – Wilaya ya Mjini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Mwinyi amemuelezea Marehemu Charles Hilary kuwa ni mchapakazi, mcheshi, mtu wa watu, na mzalendo wa kweli aliyeipenda nchi yake kwa dhati.Dkt. Mwinyi amewanasihi Watendaji wa Serikali kuwa na utamaduni wa kuwasifu na kuthamini watendaji wazuri wakiwa hai, badala ya kusubiri mpaka wafariki dunia.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza kuwa Taifa lina wajibu wa kuendelea kumuenzi Marehemu Charles Hilary kwa utendaji wake uliotukuka katika dhamana alizomkabidhi wakati wa uhai wake.Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi ameifariji familia ya Marehemu Charles Hilary, akiwemo mjane wa marehemu, Sarah Mwakanjuki, na kuwataka wawe na subira na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba.

Misa ya kumuombea marehemu imefanyika katika Kanisa Kuu la Anglikana, Mkunazini.Akitoa salamu za familia, Mtoto wa marehemu, Faith Charles Hilary, ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa heshima kubwa aliyopewa Marehemu Charles Hilary wakati wa uhai wake, kwa kumuamini katika nyadhifa muhimu Serikalinina kumuaga kwa heshima baada ya kifo chake.

Marehemu Charles Hilary alifariki dunia tarehe 11 Mei 2025 akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Mlonganzila, Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu. Ameacha mjane na watoto wawili.

spot_img

Latest articles

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...

KAIMU MSAJILI TPRB ASHIRIKI MAFUNZO ELEKEZI YA UONGOZI KWA WATENDAJI WAKUU WA TAASISI, MASHIRIKA YA UMMA NA WAKALA ZA SERIKALI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji (TPRB),...

More like this

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...