Rais Mwinyi: Tutamuenzi Charles Hilary kwa utendaji wake uliotukuka

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewaongoza Viongozi mbalimbali na mamia ya Wananchi katika maziko ya Marehemu Charles Martin Hilary, aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu.

Mapema, Rais Dkt. Mwinyi aliwaongoza Viongozi na Wananchi katika Ibada ya kuuaga mwili wa marehemu, iliyofanyika katika Viwanja vya Mapinduzi Square, Michenzani – Wilaya ya Mjini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Mwinyi amemuelezea Marehemu Charles Hilary kuwa ni mchapakazi, mcheshi, mtu wa watu, na mzalendo wa kweli aliyeipenda nchi yake kwa dhati.Dkt. Mwinyi amewanasihi Watendaji wa Serikali kuwa na utamaduni wa kuwasifu na kuthamini watendaji wazuri wakiwa hai, badala ya kusubiri mpaka wafariki dunia.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza kuwa Taifa lina wajibu wa kuendelea kumuenzi Marehemu Charles Hilary kwa utendaji wake uliotukuka katika dhamana alizomkabidhi wakati wa uhai wake.Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi ameifariji familia ya Marehemu Charles Hilary, akiwemo mjane wa marehemu, Sarah Mwakanjuki, na kuwataka wawe na subira na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba.

Misa ya kumuombea marehemu imefanyika katika Kanisa Kuu la Anglikana, Mkunazini.Akitoa salamu za familia, Mtoto wa marehemu, Faith Charles Hilary, ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa heshima kubwa aliyopewa Marehemu Charles Hilary wakati wa uhai wake, kwa kumuamini katika nyadhifa muhimu Serikalinina kumuaga kwa heshima baada ya kifo chake.

Marehemu Charles Hilary alifariki dunia tarehe 11 Mei 2025 akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Mlonganzila, Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu. Ameacha mjane na watoto wawili.

spot_img

Latest articles

Aliyekuwa akiombewa amuua mchungaji wake kwa panga

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linamshikilia Victor Fransis Thomas (39), mkulima...

Lissu awaambia wafuasi wake wajiandae akitoka ni mchakamchaka

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Chama Cha  Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amewaambia wasuasi na...

Wafanyakazi wa Majumbani 700 Watunukiwa Vyeti vya Mafunzo ya VETA

Na Tatu Mohamed ZAIDI ya wafanyakazi wa majumbani 700 wamepatiwa mafunzo maalum na kutunukiwa vyeti...

Kada wa CCM, Lameck Nyambara Ajitosa Ubunge Segerea

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lameck Nyambara amechukua fomu ya kuwania Ubunge Jimbo...

More like this

Aliyekuwa akiombewa amuua mchungaji wake kwa panga

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linamshikilia Victor Fransis Thomas (39), mkulima...

Lissu awaambia wafuasi wake wajiandae akitoka ni mchakamchaka

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Chama Cha  Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amewaambia wasuasi na...

Wafanyakazi wa Majumbani 700 Watunukiwa Vyeti vya Mafunzo ya VETA

Na Tatu Mohamed ZAIDI ya wafanyakazi wa majumbani 700 wamepatiwa mafunzo maalum na kutunukiwa vyeti...