G. 55 rasmi wajitoa Chadema

Na Mwandishi Wetu

Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu na wanachama wengine wa chama hicho wametangaza kujitoa katika chama hicho kwa madai ya kutoridhishwa na yanayoendelea.

Wametangaza uamuzi huo leo Mei 7, 2025 jijini Dar es wakati wakizungumza na waandishi wa habari.

Akitangaza uamuzi huo aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara, Benson Kigaila akiwa pamoja na Salumu Mwalimu, aliyewai kuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake (Bawacha), Catherine Ruge, John Mrema na Julius Mwita, amesema wamejitoa lakini hawaendi CCM.

Kigaila amesema muda ukifika wataeleza ni wapi wanapohamia na sasa wanashauriana na vyamba mbalimbali.

“Sisi tumeamua wote kwa pamoja kujiondoa Chadema ili tuwaachie hicho chama waendeshe wanavyotaka. Hatuwezi kuwa wanachama wa chama ambacho maamuzi yake hayafanywi kwa vikao.

“Hatuwezi kuwa wanachama ambao wanabaguliwa.Katiba haifuatwi, sisi sio chawa, sisi tunajitambua, tuliingia Chadema malengo na tunatoka Chadema kwa sababu malengo yameisha basi tunawaachia chama chao,” ameelaza Kigaila.

Kwa upande wake Mwalimu amesema alikuwepo katika chama hicho kwa muda mrefu na hakufuata vyeo wala fedha bali aliamini kwamba kama mtoto wa Taifa hili ana kila sababu ya kutoa mchango wake nchini.

spot_img

Latest articles

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

More like this

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...