Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Viongozi wa Serikali za vijiji wahimizwa kuweka uwazi walengwa wa TASAF

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema ni jukumu la Watendaji wa Serikali za Vijiji kuwatambua wananchi ambao wanastahili kuingizwa kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kupitia mikutano ya vijiji ili kuwepo na uwazi pamoja na kuondoa malalamiko kutoka kwa wananchi ambao wana vigezo vya kuingizwa.             

Kikwete ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi na walengwa wa TASAF wa Kata ya Masaki, Kijiji cha Kisanga Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.

Kikwete amesema kuwa, kuna baadhi ya wananchi ambao wanastahili kuingizwa kwenye mradi wa TASAF wenye sifa na vigezo lakini kutokana na kutoitishwa mikutano ya kijiji hupelekea baadhi yao kukosa nafasi ya kuingizwa kwenye mradi huo, hivyo amewataka viongozi hao kuendesha mikutano ya mara kwa mara ili kuondoa malalamiko ambayo yanaweza kutokea.

Aidha, Kikwete amesisitiza wananchi kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kwani amekuwa akijitahidi kuboresha maisha ya wananchi wake kwa maendeleo ya Taifa la Tanzania.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete anaendelea na ziara ya kikazi katika Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao pamoja na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...