Derby ya wanawake kesho, ubabe ubabe

Na Winfrida Mtoi

Simba Queens na Yanga Princess kesho Machi 18,2025 zinashuka dimbani katika mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara, kwenye Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kila mmoja akionekana kuwa na hamu ya  kuondoka na alama zote tatu ambapo Yanga Princess inahitaji kulipa kisasi ya kipigo cha bao 1-0 ilichopokea katika mechi ya mzunguko wa kwanza, huku Simba Queens ikitaka kuendeleza ubabe mbele ya wadada hao wa Jangwani.

Simba Queens ambayo ni mwenyeji wa mchezo huo, inaongoza katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 34 wakati Yanga ikiwa nafasi ya tatu na alama 24 zote zikicheza mechi 12.

Akizungumzia mchezo huo kocha mkuu wa Simba Queens, Yussif Basigi amesema ni mechi muhimu kwao kutokana na kila mmoja kuitolea macho, huku akihitaji ushindi ili kuendelea kukaa kileleni kwa sababu wamepishana alama mbili na JKT Queens iliyopo nafasi ya pili.

Kwa upande wake kocha mkuu wa Yanga Princess, Edna Lema, ametamba kuwa licha ya wapinzani wao kuwa kwenye ubora na kuongoza ligi lakini  wamejiandaa vizuri na hawana presha.

spot_img

Latest articles

Waogeleaji wa Lake Victoria Sports Club waahidi kuing’arisha Tanzania Kimataifa

Na Mwandishi Wetu Jumla ya waogeleaji sita  chipukizi wa Lake Victoria Sports Club  ya jijini...

Mbunge Kimei kinara kuzungumzia mahitaji ya wananchi

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Dkt Charles Stephen Kimei ametajwa kuwa...

Sekta binafsi zatakiwa kushiriki kikamilifu kutekeleza mikakati mbalimbali ya nchi

Na Tatu Mohamed, Mwanza  NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Stanislaus Nyongo...

Kafulila: Hatuwezi kujenga uchumi wa nchi bila kushirikisha sekta binafsi

Na Tatu Mohamed, Mwanza MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma...

More like this

Waogeleaji wa Lake Victoria Sports Club waahidi kuing’arisha Tanzania Kimataifa

Na Mwandishi Wetu Jumla ya waogeleaji sita  chipukizi wa Lake Victoria Sports Club  ya jijini...

Mbunge Kimei kinara kuzungumzia mahitaji ya wananchi

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Dkt Charles Stephen Kimei ametajwa kuwa...

Sekta binafsi zatakiwa kushiriki kikamilifu kutekeleza mikakati mbalimbali ya nchi

Na Tatu Mohamed, Mwanza  NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Stanislaus Nyongo...