Watu watatu wafariki kwa ajali Kimara Stop Over

Na Mwandishi Wetu

WATU watatu wafariki na wengine wamejeruhiwa kwenye ajali iliyotokea usiku wa kuamkia Februari 14,2025 katika Mtaa wa Kimara Stop Over.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema ajali imehusisha lori lililohama njia na kuparamia kituo cha bodaboda kilichopo Kimara Stop Over.

Amesema Lori hilo lilikuwa likitokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam na katika ajali hiyo hadi saa 9:00 alfajiri miili mitatu iliyokuwa imekandamizwa na kontena la lori hilo imeshatolewa.

“Miili ya watu hawa inasemekana walikuwa madereva pikipiki, pia tumefanikiwa kutoa pikipiki ambazo kwa idadi ni nyingi kuliko watu tuliowakuta kwa mantiki hiyo taarifa ya Polisi itaweka bayana,” amesema Chalamila.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, RPC Mtatiro Kitinkwi amesema kutokana na idadi ya pikipiki kuwa kubwa kuliko miili iliyokutwa, inawezekana wakati wa tukio watu walikimbia kujiokoa.

“Taarifa kwa kirefu tutaitoa tukishajua chanzo cha ajali hii kwa kuwa imetokea usiku na tumekuwa hapa kwa zaidi ya saa mbili,” amesema Kamanda Kitinkwi.

Baadhi ya mashuhuda wanasema gari hilo lilifeli brake na kukwepa daladala zilizokuwa zimebaki kwenye zebra na kuangukia watu waliokuwa wamesimama pembezoni mwa barabara pamoja na pikipiki 15, zilizokuwa zimeegeshwa kwenye eneo hilo.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...