Uhuru atoa wito kwa viongozi kuwasikiliza wananchi

Nairobi, Kenya

Rais wa zamani wa Kenya Uhuru Kenyatta, ametoa wito wa amani kufuatia maandamano ya kupinga Muswada wa Fedha wa 2024 ambayo siku ya Jumanne yalikumbwa na matukio ya vurugu baada ya waandamanaji kuvamia Bunge la Taifa.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Uhuru alielezea masikitiko yake kuhusu Wakenya waliouawa wakati wa maandamano, akisisitiza umuhimu wa viongozi waliochaguliwa kuwasikiliza waliowapigia kura.

“Wakati huu wa majaribu, nataka kuwakumbusha viongozi wote kwamba walichaguliwa na wananchi. Kuwasikiliza wananchi si chaguo bali ni wajibu uliowekwa katika misingi ya katiba yetu na katika misingi ya demokrasia,” alisema.

Uhuru, aliongeza kuwa serikali haifai kutumia nguvu na kuwa na upinzani dhidi ya Wakenya wanaotekeleza haki zao za kikatiba kwa maandamano ya amani.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...