Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu

KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo Machi 4, 2026, ametembelea Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) kwa ziara ya kujitambulisha kufuatia kuteuliwa kwake na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kushika wadhifa huo.

Ziara hiyo ya Dk. Msemwa, aliyeteuliwa kushika wadhifa huo Februari 6, 2026, ilianza kwa mapokezi rasmi OMH, jijini Dar es Salaam, ikifuatiwa na utambulisho wa menejimenti.

Dkt. Msemwa alitembelea maeneo mbalimbali ya kazi na kujionea mazingira ya utendaji pamoja na mifumo inayotumika katika kusimamia uwekezaji wa Serikali na rasilimali za umma.

Katika kikao cha pamoja na menejimenti, alipokea wasilisho la kina lililoelezea muundo wa taasisi, majukumu ya kisheria, utekelezaji wake, mafanikio yaliyopatikana na mipango ya muda mrefu ya kimkakati.

Wasilisho hilo lilibainisha mchango wa taasisi za umma katika kuongeza mapato ya Serikali, kuimarisha nidhamu ya matumizi na kuongeza tija katika uwekezaji wa umma.

Akizungumza baada ya wasilisho hilo, Dkt. Msemwa aliipongeza Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa utendaji mzuri na mageuzi yanayoendelea, hususan katika kuimarisha mchango wa taasisi za umma katika uchumi wa taifa.

Alisisitiza usimamizi madhubuti wa rasilimali za umma, uwazi, na uwajibikaji kama misingi ya kujenga uchumi imara na endelevu.

Aidha, aliahidi ushirikiano wa karibu katika kutatua changamoto zozote zinazoweza kuathiri utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo.

Kwa upande wake, Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, ambaye alikuwa mwenyeji wa ziara hiyo, alimshukuru Katibu Mkuu kwa kutenga muda wa kutembelea ofisi hiyo.

Alieleza kuwa ziara hiyo ni ishara ya kuimarisha mshikamano wa kiutendaji na mawasiliano ya moja kwa moja kati ya taasisi.

Bw. Mchechu aliahidi kutoa ushirikiano wowote utakaohitajika ili kuhakikisha kila taasisi inatekeleza wajibu wake kwa ufanisi, akisisitiza kuwa kujenga wizara imara kunaanzia katika kuzijenga taasisi zilizo chini yake kuwa imara, zenye uwajibikaji na zinazozingatia matokeo.

Alibainisha kuwa ushirikiano wa karibu kati ya Ofisi ya Rais – Uwekezaji na Ofisi ya Msajili wa Hazina utaongeza ufanisi wa usimamizi wa uwekezaji wa Serikali na kulinda maslahi ya taifa.

Ziara hiyo imeimarisha mahusiano ya kikazi na kuweka msingi wa ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuongeza tija, uwazi na mchango wa taasisi za umma katika maendeleo ya kiuchumi ya Tanzania.

spot_img

Latest articles

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

More like this

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...