Mzee miaka 63 kizimbani kwa kumbaka binti yake

Na Malima Rubasha, Serengeti

Mahakama ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, imempandisha kizimbani Marwa Masegwe(63) mkazi wa Kijiji cha Kibeyo Kata ya Kisangura kwa kosa la kumbaka binti yake wa kuzaa mwenye umri wa miaka 10 usiku Mei 15 na 16,2024 maeneo ya nyumbani kwake.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Joseph Mohere, akisoma hati ya mashtaka ameiambia mahakama hiyo kuwa katika kesi jinai namba 14565 ya mwaka 2024, mshtakiwa Marwa Mwita Masegwe mwenye umri wa miaka 63 mkazi wa kijiji cha kibeyo wilayani Serengeti alimbaka binti wa miaka 10 ambaye ni mtoto wake wa kuzaa, siku ya Mei 15 na 16 mwaka huu majira ya usiku nyumbani kwake katika kijiji cha kibeyo.

Hakimu Mohere aliendelea kuieleza mahakama kuwa hali hiyo ilipelekea binti huyo(jina limehifadhiwa) kutoa taarifa kwa majirani ili apate msaada kuhusu kitendo alichofanyiwa na baba yake kwa kuwa walikuwa wanaishi yeye na mdogo wake wa kiume na baba yao mzazi bila kuwepo kwa mzazi mwingine.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Nico Malekela pamoja na Paul Mlelwa umedai kuwa upande wa Jamhuri una mashahidi wanne na kati yao mashahidi watatu ni kutoka Ofisi ya Ustawi wa Jamii Wilaya ya Serengeti, Mganga kutoka hospitali ya Wilaya na Mhanga mwenyewe ambaye ni binti huyo na kwamba mashahidi wametoa ushahidi pasipo shaka yoyote.

Hata hivyo kwa upande wa mshtakiwa alipotakiwa kujitetea dhidi ya kesi hiyo inayomkabili alikana kuhusika kutenda kosa hilo.

Shauri hilo limeahairishwa hadi Juni 17, 2024 hadi kesi itakapotajwa tena na mshtakiwa amerudishwa rumande.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...