Na Mwandishi Wetu
SIMBA imechukua alama zote tatu kwa Fountain Gate kufuatia ushindi wa 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa dimba la Sheikh Amri Abeid, Arusha.
Katika mchezo ulichezwa leo Aprili 15,2026 mabao ya Simba yamefungwa na Clatous Chama (dk 45+6), Libase Gueye (dk 53) na Shaban Pandu (dk71).

Mchezo huo ulianza kwa kasi huku Fountain Gate wakijaribu kuzuia mashambulizi ya Simba, lakini ukuta wao ulipasuka dakika za nyongeza kabla ya mapumziko:
Ushindi huo unamfanya Mnyama Simba kufikisha pointi 39 baada ya mechi 18 akiendelea kusalia nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi hiyo, akiwa alama tano nyuma ya vinara Yanga.


