Na Mwandishi Wetu
ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi kwa vijana wadogo ‘East Africa Development Swimming Gala’ yatakayoanza Aprili 18 hadi 19, 2026 katika bwawa la Shule ya Sekondari ya FK iliyopo Jijini Dar es Salaam.
Mashindano hayo yaliyondaliwa na Prime Sports Agency yatakayoshirikisha nchi tano ambazo ni Kenya, Uganda, Malawi, Rwanda, Burundi pamoja na wenyeji Tanzania.
Akizungumzia mashindano hayo, Mkurugenzi wa Mipango wa Prime Sports Agency, Jeremiah Keema, amesema kuwa lengo ni kutoa nafasi kwa wavulana na wasichana kutoka shule na vilabu mbalimbali kushindana, kuonesha vipaji vyao na kuvikuza.
“Mashindano hayo yanatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya mchezo wa kuogelea kwa vijana na kuibua vipaji vipya vya kimataifa,”


