Mchezaji auawa na majambazi nchini Ghana

MCHEZAJI wa soka nchini Ghana, Dominic Frimpong, ameuawa kwa kupigwa risasi baada ya jana Jumapili usiku  na majambazi wenye silaha kushambulia basi la timu yake ya Berekum Chelsea.

Tukio hilo lilitokea katika barabara ya Goaso–Bibiani wakati timu ikirejea nyumbani baada mchezo wa ya Ligi Kuu ya Ghana dhidi ya Samartex katika mji wa Samreboi kusini mwa Ghana.

 Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika klabu hiyo, majambazi hao walifunga barabara na kuanza kulishambulia basi lilikuwa limebeba viongozi na wachezajiwakati dereva akijaribu kurudi nyuma.

 Jeshi la Polisi nchini humo limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema Frimpong alifariki  wakati akipatiwa matibabu hospitalini kutokana na majeraha ya risasi.

 Chama cha Soka nchini Ghana(GFA) katika taarifa yake iliyotoa leo Jumatatu Aprili 13,2026, kimesema kimepokea taarifa hiyo kwa mshtuko mkubwa, huku kikimueleza  mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 kuwa mwenye kipaji na mapenzi ya mchezo huo.

 Timu hiyo imekumbwa na mkasa huo wakati  ilipokuwa ikirejea kutoka  kwenye mchezo wa Ligi  Kuu ya Ghana dhidi ya Samaetex huko  Samreboi. Umbali wa kilomita 270 kutoka Berekum.

spot_img

Latest articles

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...

Taasisi za umma zatakiwa kuachana na utendaji wa mazoea ili kufanikisha Dira 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana...

More like this

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...