Minziro akabidhiwa Fountain Gate FC

Na Mwandishi Wetu

KLABU ya Fountain Gate FC imemtangaza Fred Felix Minziro kuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, akichukua nafasi ya Mohamed Laizer ambaye amefutwa kazi kutokana na mwenendo usioridhisha wa timu.

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo, Minziro ataongoza benchi la ufundi akisaidiwa na makocha  wengine Mathias Wandiba pamoja na Abubakari Francis, ambaye anaendelea na majukumu yake ndani ya kikosi hicho.

Minziro anapewa jukumu hilo wakati Fountain Gate ikiwa katika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kucheza michezo 17 na kujikusanyia alama 16.

Uongozi wa klabu hiyo umesema  una Imani na Minziro kutokana na uzoefu wake katika soka la Tanzania, huku ikiendelea kuhakikisha inajenga timu imara.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...