Vunjabei, Sara kuisaka heshima ya Tanzania One ulingoni

Na Winfrida Mtoi

MABONDIA wa ngumi za kulipwa, Halima Ramadhani maarufu Vunjabei na Sara Alex wanatarajia kupanda ulingoni Machi 21, 2026 kusaka heshima ya Tanzania One katika pambano litakalopigwa Uwanja wa Kinesi, Dar es Salaam.

Siku hiyo imeandaliwa maalumu kwa ajili ya kusherehekea maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani, kutakuwa na mapambano mengi yatakayowakutanisha mabondia mbalimbali kutoka mikoa tofauti.

Akizungumzia maandalizi ya pambano hilo lililopewa jina la Punch kwa Heshima, Halima amesema yeye ni bondia mkubwa, amecheza na mabondia wengi wakubwa hivyo hana hofu na mpinzani wake.

“Huwa sina show mbovu, mabondia wa kike Tanzania wananielewa vizuri, nimepigana nchi kibao nimekutanza na changamoto nyingi nje ya nchi na Watanzania wanaijua kazi yangu. Sara Alex anajua anakwenda kucheza na bondia mkubwa,” ametamba.

Amejinasibu kuwa katika uzoefu wake wa masumbwi amecheza na mabondia wakali wa nje ya nchi na amewahi kutwaa ubingwa wa WBF nchini Ujerumani, ameshinda pambano Afrika Kusini, hivyo hakuna ninachomzuia kupiga mpinzani wake.

spot_img

Latest articles

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

Mufti Zubeir asisitiza upendo, kupuuza wanaoneza chuki za kidini mtandaoni

Na Mwandishi Wetu MUFTI na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally ametoa...

More like this

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...