Msimu wa pili mbio za Pande Marathon kuzinduliwa Feb 14 Siku ya Wapendanao

Na Mwandishi Wetu

UZINDUZI wa mbio za Msakuzi Pande Game Reserve Marathon awamu ya pili, zinazofanyika ndani ya Pori la Akiba la Pande, unatarajia kufanyika Februari 14, 2026 siku ya Wapendanao (Valentine Day).

Uzinduzi huo unaondaliwa na Msakuzi Sports Promotion, unatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Forest Park Kamsuti, uliopo Mbezi Msakuzi, jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa Msakuzi Sports Promotion Filbert Mosha amewaambia Waandishi wa Habari kwamba siku ya uzinduzi kutakuwa na burudani ya bendi maalum ya muziki, vinywaji, nyama choma na shangwe nyingine.

“Tutakuwa na mgeni rasmi ambaye tutamtangaza baadaye. Lakini pia siku hiyo tutapata mrejesho na ushuhuda wa msimu uliopita, kutakuwa na surprise kwa Wapendanao, bendi itakuwa live kuanzia saa sita mchana hadi majogoo, kwa kifupi tutakuwa na uzinduzi wa kishindo ambao haujapata kutokea,” alisisitiza Mosha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Msakuzi Sports Promotion, Dk. John Kisimbi alisema utakuwa uzinduzi wa aina yake hivyo wananchi wasipange kukosa.

“Mwaka jana ambao ulikuwa msimu wa kwanza, tulifanikiwa sana, washiriki zaidi ya 500 walijitokeza na baada ya mbio walipata burudani mbalimbali ya live bendi, nyama choma za pori, walipata fursa ya kuangalia wanyama na hakuna aliyetaka kuondoka, msimu huu wa pili mambo ni moto zaidi.

“Jambo kubwa ni kwamba siku ya Wapendanao, tutazindua rasmi msimu wa pili wa maandalizi ya mbio hizo kwenye ukumbi wa Forest Park Kamsuti,” alisema Dk. Kisimbi.

Aliishukuru Mamlaka ya Usimamizi ya Wanyama Pori Tanzania (TAWA) kwa kuridhia Pande Marathon kufanyika ndani ya hifadhi hiyo kama sehemu ya kukuza utalii wa Pande na msimu huu wa pili wanatarajia kuwa na washiriki zaidi 2000.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...