Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi

KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna mechi rahisi ya Ligi Kuu, lakini wamejipanga kuhakikisha wanachukua pointi katika mchezo wao wa kesho dhidi ya KMC utakaopigwa saa 1:00 usiku kwenye Uwanja wa KMC Complex, Mwenye jijini Dar es Salaam.

Barker amesema anawaheshimu wapinzani, lakini  wamejiandaa na wachezaji wake wanaonekana kujitoa kwa kila mechi na kiwango cha timu kinaendelea kuimarika kila mchezo pamoja na wachezaji wengi wapya.

Amesema baada ya mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika walirejea kufanya maandalizi mchezo wa kesho ambao ni muhimu kwao kupata ushindi ili kuimarisha nafasi yao katika msimamo wa Ligi Kuu.

“Maandalizi yanakwenda vizuri hadi sasa, tunahitaji kucheza mechi hii vizuri ili kupata ushindi unaotakiwa kama malengo yetu tulijiwekea,” amesema kocha huyo.

Kwa upande wake Kocha Mkuu wa KMC, Mohamed Abdallah ‘Bares’ amesema wanajua wanakwenda kucheza mchezo mkubwa, pia bado wana presha kutokana na kuwa katika hali ya chini kwa sababu ya kushindwa kupata matokeo mazuri,

 “Kesho tunaingia kwa kutuliza presha kwa mashabiki paamoja na wachezaji wetu, naamini presha itaondoka kutokana na matokeo tutakayopata katika mchezo huo. Kikubwa ni wachezaji kuwa makini,” amesema Bares.

Katika msimamo wa ligi hiyo Simba ipo nafasi ya saba na pointi 16, ikicheza mechi saba, wakati KMC  inaburuza mkia na  pointi nane ilizokusanya katika michezo 14, ikishinda mechi mbili pekee hadi sasa.

spot_img

Latest articles

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

IAEA yaipongeza Zanzibar kwa Ushirikiano Katika Kilimo na Mifugo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Suleiman Masoud Makame,...

Wakurugenzi Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa kushirikiana na Taasisi ya...

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...

More like this

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

IAEA yaipongeza Zanzibar kwa Ushirikiano Katika Kilimo na Mifugo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Suleiman Masoud Makame,...

Wakurugenzi Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa kushirikiana na Taasisi ya...