Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa, ametoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali ya gari mkoani Iringa walipokuwa wakirejea nyumbani wakitokea kuripoti Maadhimisho ya Miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mndolwa, akiwa ameambatana na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa NIRC, Mariam Mziwanda, alifika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa na kuwatembelea waandishi hao wa habari, ambapo aliwajulia hali na kuwapa pole kwa niaba ya taasisi hiyo.

Ajali hiyo ilitokea jana, Februari 5, 2026, katika Kata ya Idodi, Wilaya ya Iringa Vijijini.

Gari lililohusika katika ajali hiyo lilikuwa limewabeba Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Joseph Nzala Lyata, pamoja na waandishi wa habari akiwemo Frank Leonard, Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa na mwandishi wa magazeti ya Habari Leo na Daily News.

Waandishi wengine waliopata ajali hiyo ni pamoja na Zuhura Zukheriwa wa Abood TV, Denis Mlowe wa blogu ya Fullshangwe, Clemence Sanga wa Channel Ten pamoja na Herieth Mola wa Mkombozi Online TV.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

More like this

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...