Simba yataka Polisi iwashughulikie waliomkashfu bosi

Na Mwandishi Wetu

KLABU ya Simba imeliandikia barua Jeshi la Polisi  ili kuwachukulia hatua za kisheria wanachama na mashabiki wa klabu hiyo  waliohusika na mkutano wa kutoa kashfa na maneno yasio ya staha kwa mwekezaji wao Mohamed Dewji (Mo).

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Klabu hiyo, Bodi ya Wakurugenzi ya Simba imesikitishwa na vitendo hivyo na kutaka wote waliohusika au kula njama za kuandaa mkutano huo  kufikishwa katika vyombo vya dola kwa makosa ya jinai.

“Bodi inasisitisha kuwa haitabariki wala kuvumilia mtu yoyote anayeharibu taswira ya klabu kwa namna yoyote ile,” imesema taarifa hiyo.

Aidha uongozi wa Simba, umetoa onyo kwa baadhi ya wanachama na mashabiki wa klabu hiyo wanaotumia nembo rasmi ya klabu bila kupata ruhusa ya moja kwa moja kutoka kwa ngazi za juu za klabu hiyo.

Umetoa wito kwa wanachama na mashabiki kuzingatia taratibu rasmi za klabu na kushirikiana kwa pamoja katika kuendeleza heshima na hadhi ya klabu.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...