Mukwala atua Zanzibar, Simba ikiivaa Azam kesho Mapinduzi Cup

Na Winfrida Mtoi

WAKATI Simba kitarajia kukabiliana na Azam FC kesho katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya kombe la Mapinduzi, mshambuliaji wa timu hiyo raia wa Uganda Steven Mukwala  amejiunga kikosi hicho  leo na kufanya mazoezi ya mwisho na wenzake.

Mukwala   amerejea kikosini baada ya kumaliza majukumu katika timu ya taifa ya Uganda iliyokuwa ikishiriki fainali za kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2025) ambapo waliishia hatua ya makundi.

Simba imefanya mazoezi ya mwisho katika mazoezi ya mwisho leo Januari 7, 2026 kwenye viwanja vya Maisara, Unguja kujiandaa na mechi hiyo itakayochezwa kesho Alhamisi Januari 8, 2026 kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, saa 2:15 usiku.

Kuelekea mchezo huo, makocha wa timu hizo mbili zenye upinzani mkali katika Ligi Kuu Tanzania, Steve Barker wa Simba na Florent Ibenge Azam FC wamezungumzia maandalizi yao kuelekea mchezo huo mbele ya waandishi wa habari, huku mmoja  akijivunia kikosi chake.

Kocha wa Simba Barker amesema wachezaji wake wana morali ya hali ya juu na wameongezeka kikosini tofauti na walivyoanza, hivyo wamejipanga kucheza vizuri  kuhakikisha wanashinda mchezo huo ili kutinga fainali ikiwezekana kuchukua taji hilo.

Naye kocha mkuu wa Azam FC, Ibenge ameeleza kuwa  anaiheshimu Simba ni kubwa na bora lakini malengo yao katika mechi hiyo ni kuondoka na ushindi.

spot_img

Latest articles

Tuna deni la kusimamia miradi na kusikiloza kero za wananchi ili kuleta Maendeleo ya kweli: Salome

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa...

2025 mwaka wa mageuzi na matokeo katika mashirika ya umma

Na Mwandishi Wetu MWAKA 2025 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa Ofisi ya Msajili wa...

Wakatoliki feki wamechafua hali ya hewa, aibu hii anabeba nani?

TAHARUKI kubwa imeibuka nchini. Unaweza kuiona ukichungulia kwenye mitandao ya kijamii. Imesababishwa na akili...

Serikali yawekeza zaidi ya Sh. Bilioni 280 kuimarisha upatikanaji umeme Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano...

More like this

Tuna deni la kusimamia miradi na kusikiloza kero za wananchi ili kuleta Maendeleo ya kweli: Salome

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa...

2025 mwaka wa mageuzi na matokeo katika mashirika ya umma

Na Mwandishi Wetu MWAKA 2025 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa Ofisi ya Msajili wa...

Wakatoliki feki wamechafua hali ya hewa, aibu hii anabeba nani?

TAHARUKI kubwa imeibuka nchini. Unaweza kuiona ukichungulia kwenye mitandao ya kijamii. Imesababishwa na akili...