Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi

LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili kupigwa ambapo Yanga na Azam zimefanikiwa kuondoka na alama tatu kila mmoja, huku Mnyama Simba akiambulia kichapo.

Yanga imeibuka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya Coastal Union kwenye dimba la Jamhuri Dodoma, wakati Azam imeipiga Simba mabao 2-0 Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Bao pekee la Yanga lilifungwa na Prince Dube dakika ya 88, huku mabao ya Azama yakifungwa na Jephte Kitambala dakika 81 na Idd Seleman ‘Nado’ dakika ya 89.

Matokeo ya Simba yamewafanya mashabiki wake waondoke uwanjani kwa hasira huku wakiwatupia lawama viongozi wa klabu hiyo.

Kocha wa Simba Selemani Matola ametaja kile kilichowaangusha kuwa ni kupoteza umakini kwa wachezaji wake dakika za jioni.

Kwa upande wake kocha wa Azam FC, Florent Ibenge amesema mchezo ulikuwa mgumu lakini mabadiliko aliyofanya kipindi cha pili yamempa matokeo mazuri.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

More like this

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...