Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi

LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili kupigwa ambapo Yanga na Azam zimefanikiwa kuondoka na alama tatu kila mmoja, huku Mnyama Simba akiambulia kichapo.

Yanga imeibuka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya Coastal Union kwenye dimba la Jamhuri Dodoma, wakati Azam imeipiga Simba mabao 2-0 Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Bao pekee la Yanga lilifungwa na Prince Dube dakika ya 88, huku mabao ya Azama yakifungwa na Jephte Kitambala dakika 81 na Idd Seleman ‘Nado’ dakika ya 89.

Matokeo ya Simba yamewafanya mashabiki wake waondoke uwanjani kwa hasira huku wakiwatupia lawama viongozi wa klabu hiyo.

Kocha wa Simba Selemani Matola ametaja kile kilichowaangusha kuwa ni kupoteza umakini kwa wachezaji wake dakika za jioni.

Kwa upande wake kocha wa Azam FC, Florent Ibenge amesema mchezo ulikuwa mgumu lakini mabadiliko aliyofanya kipindi cha pili yamempa matokeo mazuri.

spot_img

Latest articles

Zawadi ya gari yawapa mzuka mabondia

Na Winfrida Mtoi Waandaaji wa pambano la Dar Boxing Derby wameweka gari aina ya Crown...

Nani anajali kurejesha hadhi Tanzania?

WIKI iliyopita haikuwa ya habari njema kwa Taifa la Tanzania huko duniani. Pamoja na...

TCAA YAIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA DAWATI MAALUM

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia kwa Mkurugenzi wake...

TBA YASHINDA TUZO YA BANDA BORA SABASABA, YATANGAZA DIRA YA KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umeibuka mshindi wa pili na kutunukiwa tuzo...

More like this

Zawadi ya gari yawapa mzuka mabondia

Na Winfrida Mtoi Waandaaji wa pambano la Dar Boxing Derby wameweka gari aina ya Crown...

Nani anajali kurejesha hadhi Tanzania?

WIKI iliyopita haikuwa ya habari njema kwa Taifa la Tanzania huko duniani. Pamoja na...

TCAA YAIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA DAWATI MAALUM

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia kwa Mkurugenzi wake...