Dkt Msonde: Uhandisi wa Tanzania uko mikononi mwa vijana

Na Tatu Mohamed

NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, amewataka wahandisi vijana nchini kutumia ubunifu na maarifa yao kutafuta suluhisho za changamoto zinazolikabili taifa badala ya kusubiri kupatiwa majibu kutoka nje.

Akizungumza leo Septemba 24, 2025 wakati akifunga Kongamano la Pili la Vijana Wahandisi (YEF) lililoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi Tanzania (ERB), Dkt. Msonde amesema uhandisi wa Tanzania uko mikononi mwa vijana na si wageni kutoka mataifa mengine.

“Suluhisho la kiuhandisi sio kwa kuiga au kuleta kutoka mataifa mengine pekee. Hatutoweza kutatua matatizo yetu kwa kufikiria namna ile ile na utaratibu ule ule. Elimu yenu ya kiuhandisi mliyoipata ikusaidieni kuleta vitu vipya vya kutatua changamoto zetu za ndani,” amesema.

Ameongeza kuwa kongamano hilo ni jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu na kuonesha ubunifu wa vijana, akiwapongeza washiriki kwa bunifu walizozionesha.

“Mafanikio yanahitaji ujasiri, nidhamu na ushirikiano wa kimkakati. Msikate tamaa mnaposhindwa, kwani kushindwa huko ndiko ishara ya kuelekea kwenye mafanikio zaidi. Mbegu ili iote lazima ioze,” amesema Dkt. Msonde.

Kwa upande wake, Kaimu Msajili wa ERB, Wakili Mercy Jilala, amesema jumla ya wahandisi vijana 145 wameshiriki katika kongamano hilo huku 84 wakihudhuria kwa njia ya mtandao.

“Bodi iliamua kuanzisha mafunzo haya kwa sababu tuliona vijana wanapohitimu vyuoni wanakosa fursa ya kutoa mawazo mapya na kufundishwa namna ya kujiajiri. Tunawaandaa ili wasibaki kusubiri ajira pekee,” amesema.

Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhandisi Menye Manga, amesema ERB itaendelea kutoa mafunzo na makongamano ya aina hiyo kwa kuwa idadi ya wahitimu wa uhandisi inaongezeka huku changamoto za ajira zikibaki kubwa.

Kongamano hilo lililobeba kauli mbiu: “Mustakabali wa Uhandisi: Mageuzi ya Kitaifa Yanaongozwa na Suluhisho za Ubunifu za Vijana”, liliwakutanisha wahandisi vijana na watoa mada mbalimbali kwa lengo la kujenga uwezo wa kitaaluma na kuhimiza ubunifu katika sekta ya uhandisi.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...