Simbu aweka rekodi ya pekee Tanzania, Rais Samia ampongeza

Na Mwandishi Wetu

Mwanariadha Alphonce Simbu ameweka rekodi ya kuwa mwanariadha wa kwanza Tanzania  kushinda medali ya dhahabu katika mbio za riadha za Dunia 2025 (World Athletics)  za kilomita 42 zilizofanyika katika Uwanja wa Taifa wa Japan mjini Tokyo.

Alphonce Simbu alivuka mstari wa kumalizia mbele ya Mjerumani Amanal Petros na kuibuka mshindi wa kwanza akifanikiwa kutwaa medali ya dhahabu akimaliza kwa saa 2:09:4.

Medali hito ya Simbu ni ya kwanza kwa mwanariadha wa Tanzania kuwahi kushinda katika riadha.

“Nimeweka historia leo, ikiwa ni medali ya kwanza ya dhahabu ya Tanzania katika mashindano ya dunia. Nakumbuka mwaka 2017, kwenye mashindano ya dunia ya London, nilishinda shaba,” Simbu amesema baada ya ushindi wake.

Rais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan amempongeza mwanariadha huyo, kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamiii kwa kusema “Hongera sana Alphonce Simbu kwa Medali ya Dhahabu ya ushindi wa Mbio Ndefu za Mashindano ya Kimataifa ya Riadha ya Tokyo ndani ya saa 2:09:48 umeandika sehemu ya historia ya Taifa letu”

“Kama nilivyokusihi uliposhika nafasi ya pili kwenye Boston Marathon mwezi Aprili mwaka huu, ushindi wako ni matokeo ya nidhamu yako ya hali ya juu na kujituma kwa bidii kwenye kazi, umekuwa mfano bora kuhusu nguzo hizo mbili za kazi kwa wanariadha na wanamichezo wenzako na hata kwa wasiyo wanamichezo endelea kuipeperusha vyema na kuiheshimisha bendera ya Taifa letu” ameandika Dk. Samia.

spot_img

Latest articles

TANESCO YABORESHA MAISHA YA WAFANYAKAZI NYUMBA YA MUNGU

📌 Nyumba za wafanyakazi zakarabatiwa, kuboresha utendaji wa kazi 📌 Mtambo wa kisasa wa kuchakata...

KATAMBI ATOA ONYO KWA MAKUNDI YA ULINZI YASIYO RASMI

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, ametoa onyo kwa...

Watumishi OTR wapatiwa mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa Ubora

Na Mwandishi wa OTR OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imeendelea na hatua za kuimarisha...

MRADI WA UMEME MPOMVU – GGM KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI GEITA – MHE. SALOME

📌 Kukamilika kwa njia mpya kutatoa fursa kwa njia ya awali kuendelea kunufaisha wananchi...

More like this

TANESCO YABORESHA MAISHA YA WAFANYAKAZI NYUMBA YA MUNGU

📌 Nyumba za wafanyakazi zakarabatiwa, kuboresha utendaji wa kazi 📌 Mtambo wa kisasa wa kuchakata...

KATAMBI ATOA ONYO KWA MAKUNDI YA ULINZI YASIYO RASMI

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, ametoa onyo kwa...

Watumishi OTR wapatiwa mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa Ubora

Na Mwandishi wa OTR OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imeendelea na hatua za kuimarisha...