Simbu aweka rekodi ya pekee Tanzania, Rais Samia ampongeza

Na Mwandishi Wetu

Mwanariadha Alphonce Simbu ameweka rekodi ya kuwa mwanariadha wa kwanza Tanzania  kushinda medali ya dhahabu katika mbio za riadha za Dunia 2025 (World Athletics)  za kilomita 42 zilizofanyika katika Uwanja wa Taifa wa Japan mjini Tokyo.

Alphonce Simbu alivuka mstari wa kumalizia mbele ya Mjerumani Amanal Petros na kuibuka mshindi wa kwanza akifanikiwa kutwaa medali ya dhahabu akimaliza kwa saa 2:09:4.

Medali hito ya Simbu ni ya kwanza kwa mwanariadha wa Tanzania kuwahi kushinda katika riadha.

“Nimeweka historia leo, ikiwa ni medali ya kwanza ya dhahabu ya Tanzania katika mashindano ya dunia. Nakumbuka mwaka 2017, kwenye mashindano ya dunia ya London, nilishinda shaba,” Simbu amesema baada ya ushindi wake.

Rais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan amempongeza mwanariadha huyo, kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamiii kwa kusema “Hongera sana Alphonce Simbu kwa Medali ya Dhahabu ya ushindi wa Mbio Ndefu za Mashindano ya Kimataifa ya Riadha ya Tokyo ndani ya saa 2:09:48 umeandika sehemu ya historia ya Taifa letu”

“Kama nilivyokusihi uliposhika nafasi ya pili kwenye Boston Marathon mwezi Aprili mwaka huu, ushindi wako ni matokeo ya nidhamu yako ya hali ya juu na kujituma kwa bidii kwenye kazi, umekuwa mfano bora kuhusu nguzo hizo mbili za kazi kwa wanariadha na wanamichezo wenzako na hata kwa wasiyo wanamichezo endelea kuipeperusha vyema na kuiheshimisha bendera ya Taifa letu” ameandika Dk. Samia.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...