Kijana ahukumiwa jela miaka 30 kwa kubaka mzee wa miaka 80 kichakani

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani, imemhukumu Said Nawanje (20) mkazi wa Yombo Lukinga, wilayani humo, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mzee wa miaka 80.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Juni Mosi, 2025 huko Kijiji cha Yombo Lukinga, Kisarawe baada ya kumvizia bibi huyo akitoka shambani ambapo alimtishia kisu kisha kumsukuma kichakani na kumbaka.

Hukumu hiyo ya kesi namba 15006/2005 imesomwa Agosti 20, 2025 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, Simon Mosses baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri.

Hakimu Mosses alieleza kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130 (1), (2) (a) na 131 (1) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

spot_img

Latest articles

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...

Rostam aanika maono yake umiliki mpya ya NMG

Na Mwandishi Wetu MFANYABIASHARA na mwekezaji wa Tanzania, Rostam Azizi, ametangaza uwekezaji mkubwa wa kimkakati...

More like this

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...