Kijana ahukumiwa jela miaka 30 kwa kubaka mzee wa miaka 80 kichakani

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani, imemhukumu Said Nawanje (20) mkazi wa Yombo Lukinga, wilayani humo, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mzee wa miaka 80.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Juni Mosi, 2025 huko Kijiji cha Yombo Lukinga, Kisarawe baada ya kumvizia bibi huyo akitoka shambani ambapo alimtishia kisu kisha kumsukuma kichakani na kumbaka.

Hukumu hiyo ya kesi namba 15006/2005 imesomwa Agosti 20, 2025 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, Simon Mosses baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri.

Hakimu Mosses alieleza kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130 (1), (2) (a) na 131 (1) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...