Chadema yaipeleka Yanga FIFA

Na Mwandishi Wetu

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetuma barua ya malalamiko kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa(FIFA), ikilitaka kuifanyia uchunguzi klabu ya Yanga kuhusu kujihusisha na masuala ya kisiasa.

Malalamiko ya Chadema yametokana na Yanga kushiriki katika harambee ya kuchangia fedha za kufanikisha kampeni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu Oktoba 29,2025 iliyofanyika Agosti 12, 2025, ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam ambapo klabu hiyo ilichangia sh 100 milioni.

Kupitia barua hiyo, Chadema pia imeomba kuchukuliwa hatua za kinidhamu kulingana na Kanuni kwa maofisa na viongozi wa klabu hiyo waliohusika katika jambo hilo la uchangiaji kwa madai kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa kanuni na sheria za FIFA.

“Sisi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwa heshima tunawasilisha malalamiko rasmi na ombi kuhusu mwenendo wa Young African Sports Club (“Yanga”) ya Tanzania, ambapo vitendo vya hivi karibuni ni ukiukaji wa moja kwa moja wa misingi ya FIFA,”

Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Masuala ya Nje na Diaspora wa Chadema, John Kitoka amethibitisha kuandika barua hiyo na kusema tayari imepokelewa FIFA.

Hivi karibuni baada ya kuibuka mjadala juu ya Yanga kuchangia CCM kwa sababu mashaki wake wana itikadi za vyama tofauti tofauti, uongozi wa klabu hiyo ulitoa taarifa ya ufafanuzi kuwa fedha zilizotolewa katika uchangiaji huo zimetoka Taasisi ya GSM Foundation na sio za mfuko wa wanachama.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...