Doyo wa NLD achukua fomu INEC ya kuwania Urais

Na Mwandishi Wetu

MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD), Doyo Hassan Doyo, leo ameambatana na mgombea mwenza wake, Chausiku Khatibu Mohamed, kufika katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kwa ajili ya kuchukua fomu za uteuzi.

Fomu hizo za kuomba kuteuliwa kuwania nafasi ya Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha NLD zilikabidhiwa rasmi na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu, Doyo amesisitiza dhamira yake ya kupunguza matumizi makubwa ya serikali iwapo atapewa ridhaa ya kuiongoza nchi.

Ameeleza kuwa moja ya hatua atakazochukua ni kupunguza matumizi ya magari ya kifahari kwa viongozi wa umma, akisema.

“Nimekuja kuchukua fomu ya uteuzi kwa kutumia bajaji leo, kama ishara ya kuwaunga mkono vijana wanaoishi maisha ya kawaida na wanaojitahidi kujikwamua kupitia kazi zao za ujasiriamali. Wastani wa maisha yao unapaswa kueleweka na kuungwa mkono na kila mmoja wetu, kuna haja ya kupunguza matumizi serikani ili tuwaunge mkono vijana wengi zaidi.”

Kwa upande wake, Mgombea Mwenza wa Urais, Chausiku Khatibu Mohamed, amewashukuru wanachama wa NLD na Watanzania kwa ujumla kwa kuonesha imani, mshikamano na moyo wa kizalendo katika kipindi muhimu cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.

“Tunaamini kuwa kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko chanya kwa taifa letu, huku tukiweka msingi wa amani na mshikamano wa kweli. Amani ndiyo nguzo na tunu ya taifa letu. Chama cha NLD kimejipanga kufanya kampeni za kistaarabu, bila kudhalilisha wala kutweza utu wa mtu yeyote,” amesema.

spot_img

Latest articles

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

More like this

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...