Wizara ya Katiba na Sheria yasaidia kupunguza migogoro ya ardhi Nanenane

Na Tatu Mohamed

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Jabiri Shekimweri, amesema kuwa ushiriki wa Wizara ya Katiba na Sheria katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) yanayoendelea jijini Dodoma ni fursa muhimu ya kupunguza migogoro mbalimbali, hasa ya ardhi, ambayo imekuwa changamoto kubwa kwa wananchi wa mkoa huo.

Akizungumza Agosti 6, 2025, mara baada ya kutembelea banda la wizara hiyo, Shekimweri alisema kuwa huduma zinazotolewa kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia zina umuhimu mkubwa kwa jamii, ikizingatiwa kuwa bado kuna malalamiko mengi yanayohusiana na masuala ya ardhi.

“Nimefurahi sana kukuta banda la Wizara ya Katiba na Sheria linatoa huduma hii ya msaada wa kisheria lakini pia linatoa elimu. Natoa wito kwa wananchi wote wafike hapa kupata huduma na elimu ya utatuzi wa migogoro, hasa wanawake wajitokeze kwa wingi kujifunza masuala ya mirathi kwani mara nyingi wao ndio wahanga wakuu,” amesema DC Shekimweri.

Ameongeza Wizara hiyo si tu inasikiliza na kushughulikia malalamiko ya wananchi, bali pia inawapa maarifa ya haki na wajibu wao kisheria, jambo litakalosaidia kuimarisha ustawi wa jamii na mshikamano.Shekimweri pia amepongeza elimu ya Haki na Utawala Bora inayotolewa na wizara hiyo kwa wananchi, akisema ni jambo muhimu kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao.

“Tunaelekea katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu, hivyo elimu ya haki, wajibu na utawala bora ni muhimu kwa wananchi ili waweze kushiriki kikamilifu na kwa uelewa mpana katika mchakato huo wa kidemokrasia,” amesisitiza.

Wizara ya Katiba na Sheria ni miongoni mwa taasisi zinazoshiriki kikamilifu katika Maonesho ya Nanenane kwa kutoa huduma za kisheria, elimu na ushauri kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kupeleka huduma karibu na wananchi.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...