Wizara ya Katiba na Sheria yasaidia kupunguza migogoro ya ardhi Nanenane

Na Tatu Mohamed

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Jabiri Shekimweri, amesema kuwa ushiriki wa Wizara ya Katiba na Sheria katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) yanayoendelea jijini Dodoma ni fursa muhimu ya kupunguza migogoro mbalimbali, hasa ya ardhi, ambayo imekuwa changamoto kubwa kwa wananchi wa mkoa huo.

Akizungumza Agosti 6, 2025, mara baada ya kutembelea banda la wizara hiyo, Shekimweri alisema kuwa huduma zinazotolewa kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia zina umuhimu mkubwa kwa jamii, ikizingatiwa kuwa bado kuna malalamiko mengi yanayohusiana na masuala ya ardhi.

“Nimefurahi sana kukuta banda la Wizara ya Katiba na Sheria linatoa huduma hii ya msaada wa kisheria lakini pia linatoa elimu. Natoa wito kwa wananchi wote wafike hapa kupata huduma na elimu ya utatuzi wa migogoro, hasa wanawake wajitokeze kwa wingi kujifunza masuala ya mirathi kwani mara nyingi wao ndio wahanga wakuu,” amesema DC Shekimweri.

Ameongeza Wizara hiyo si tu inasikiliza na kushughulikia malalamiko ya wananchi, bali pia inawapa maarifa ya haki na wajibu wao kisheria, jambo litakalosaidia kuimarisha ustawi wa jamii na mshikamano.Shekimweri pia amepongeza elimu ya Haki na Utawala Bora inayotolewa na wizara hiyo kwa wananchi, akisema ni jambo muhimu kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao.

“Tunaelekea katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu, hivyo elimu ya haki, wajibu na utawala bora ni muhimu kwa wananchi ili waweze kushiriki kikamilifu na kwa uelewa mpana katika mchakato huo wa kidemokrasia,” amesisitiza.

Wizara ya Katiba na Sheria ni miongoni mwa taasisi zinazoshiriki kikamilifu katika Maonesho ya Nanenane kwa kutoa huduma za kisheria, elimu na ushauri kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kupeleka huduma karibu na wananchi.

spot_img

Latest articles

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...

KAIMU MSAJILI TPRB ASHIRIKI MAFUNZO ELEKEZI YA UONGOZI KWA WATENDAJI WAKUU WA TAASISI, MASHIRIKA YA UMMA NA WAKALA ZA SERIKALI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji (TPRB),...

More like this

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...