Fountain Gate FC yakwepa kushuka daraja

Na Mwandishi Wetu

Klabu ya Fountain Gate  imefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu  Tanzania Bara kwa msimu ujao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Stand United katika mchezo wa mtoano uliopigwa kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, mkoani Manyara.

Fountain Gate meshinda jumla ya mabao 5-1 katika michezo miwili ya mtoano  ya nyumbani na ugenini baada ya kushinda 3-1 katika mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga na leo wakahitimisha kwa ushindi wa 2-0 nyumbani.

Mabao ya leo yamefungwa na Elie Mkono dakika ya 51 na Edger William dakika ya 90, hivyo kuihakikishia timu hiyo nafasi ya kuendelea kusalia  kwa msimu wa 2025/2026.

Ushindi huo umeleta furaha kwa mashabiki wa  timu hiyo kutokana na  kukwepa kushuka daraja kupitia  hatua ya mtoano.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...