Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu

ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo Cha Kodi na Mjumbe wa Seneti ya Mkoa wa Dar es Salaam Mwaka 2021/2022, amechukua na kurudisha fomu ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki.

Amanzi ameingia rasmi kugombea jimbo moja na Mbunge aliyemaliza Muda wake katika Jimbo Hilo la Morogoro Kusini Mashariki, Hamisi Taletale maarufu Babu Tale.

Amanzi ambaye ndiye kijana pekee aliyechukua fomu katika jimbo hilo akiwa na maono makubwa huku akijidhatiti kuwatumika wananchi pindi atakapopata nafasi hiyo ndani ya chama.

Akizungumza mara baada ya kurejesha fomu amesema vijana ndio nguvu kazi ya taifa hivyo ameona ni muda muhimu kuweza kulitumikia taifa lake.

Amesema kutokana na utekelezaji wa ilani ya chama chini ya usimamizi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan katika majimbo mpaka nchi umepelekea kujitathimini na kuona anafaa kuweza kumsadia Rais kuisimamia na kutekeleza ilani ya chama kwa kuwatumikia wananchi.

“Kutokana na demokrasia iliyopo kwenye chama chetu imepelekea mimi kama kijana ambae nimejitathimini na kujipima lakini pia ninauzoefu wa uongozi ndani ya chama kuamua kuchukua fomu ili chama kikinipa ridhaa niweze kuwatumikia wananchi,” amesema Amanzi.

Mpaka sasa Amanzi ni kijana pekee aliyethubutu Kugombea Ubunge katika Jimbo hilo.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

Mkazi wa Magomeni Ashinda Gari Ford Ranger Kupitia Kampeni ya Tembocard ni Shwaa ya CRDB

Na Mwandishi Wetu MKAZI wa Magomeni, Rahabu Mwambene, ameibuka mshindi wa gari aina ya...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...