Esther Bulaya: Nilikuwa Chadema kwa mkopo nimerejea, CCM ni kama  Barcelona 

Na Mwandishi Wetu

Aliyekuwa Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Esther Bulaya  amesema  alikuwa Chadema kwa mkopo sasa amerejea  Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ni sawa Barcelona  au Real Madrid na wanakwenda kutengeneza kikosi cha kushinda ‘Champions League’.

Bulaya   ambaye  amerejea  CCM na kuchukua fomu ya kugombea Ubunge, Jimbo la Bunda Mjini mkoani Mara kupitia CCM, amejinasibu  mbele ya waandishi wa habari kuwa  chama alichokuwepo ni kama timu iliyoshuka daraja, hivyo amerudi kutoka kwenye mkopo.

“Unapozngumzia Chama Cha Mapinduzi  ndio Barcelona ya Tanzania, Chama Cha Mapinduzi  kimerudisha usajili kwa wachezaji wake wa Barcelona ambao waliwatuma kwa mkopo kwenye timu ya Leicester City  ambayo imeshuka daraja,” amesema Bulaya.

Ameeleza kuwa alianza  harakati  ndani ya CCM tangu akiwa  vyuoni, hivyo  ana furaha kurejea katika chama kilichomlea.

Bulaya ni miongoni mwa wabunge 19 wa Viti Maalumu wa CHADEMA ambao chama hicho kilitangaza kuwavua uanachama, lakini walisalia bungeni hadi kuhitimishwa kwa Bunge la 12 kwa amri ya mahakama.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...