Esther Bulaya: Nilikuwa Chadema kwa mkopo nimerejea, CCM ni kama  Barcelona 

Na Mwandishi Wetu

Aliyekuwa Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Esther Bulaya  amesema  alikuwa Chadema kwa mkopo sasa amerejea  Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ni sawa Barcelona  au Real Madrid na wanakwenda kutengeneza kikosi cha kushinda ‘Champions League’.

Bulaya   ambaye  amerejea  CCM na kuchukua fomu ya kugombea Ubunge, Jimbo la Bunda Mjini mkoani Mara kupitia CCM, amejinasibu  mbele ya waandishi wa habari kuwa  chama alichokuwepo ni kama timu iliyoshuka daraja, hivyo amerudi kutoka kwenye mkopo.

“Unapozngumzia Chama Cha Mapinduzi  ndio Barcelona ya Tanzania, Chama Cha Mapinduzi  kimerudisha usajili kwa wachezaji wake wa Barcelona ambao waliwatuma kwa mkopo kwenye timu ya Leicester City  ambayo imeshuka daraja,” amesema Bulaya.

Ameeleza kuwa alianza  harakati  ndani ya CCM tangu akiwa  vyuoni, hivyo  ana furaha kurejea katika chama kilichomlea.

Bulaya ni miongoni mwa wabunge 19 wa Viti Maalumu wa CHADEMA ambao chama hicho kilitangaza kuwavua uanachama, lakini walisalia bungeni hadi kuhitimishwa kwa Bunge la 12 kwa amri ya mahakama.

spot_img

Latest articles

Makamu wa Rais atoa wito uboreshaji mfumo wa fedha

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya...

Kihongosi aahidi kutekeleza alichoagizwa na Rais Samia  Arusha

Na Mwandishi Wetu  Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha,  Kenani Kihongosi amesema  atafanya kazi aliyotumwa na Rais...

Rais Mwinyi aipongeza Yanga, aizawadia  milioni 100

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali...

Israel Salufu wa CCM achukua fomu ya kuwania Jimbo la Kilolo

Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu Israel Johaness Salufu amechukua fomu kuwania nafasi ya...

More like this

Makamu wa Rais atoa wito uboreshaji mfumo wa fedha

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya...

Kihongosi aahidi kutekeleza alichoagizwa na Rais Samia  Arusha

Na Mwandishi Wetu  Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha,  Kenani Kihongosi amesema  atafanya kazi aliyotumwa na Rais...

Rais Mwinyi aipongeza Yanga, aizawadia  milioni 100

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali...