Kaboyoka ajiunga rasmi na ACT Wazalendo

Na Tatu Mohamed

MBUNGE wa Viti Maalum wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha 2020 hadi 2025, Nagy Livingstone Kaboyoka, amejiunga rasmi na Chama cha ACT Wazalendo.

Hafla ya mapokezi imefanyika leo katika Ukumbi wa Hakainde Hichilema uliopo Makao Makuu ya ACT Wazalendo, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Kaboyoka amepokelewa na Kiongozi wa Chama hicho, Ndugu Dorothy Semu, pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wa Ngome ya Wanawake wa ACT Wazalendo.

Kaboyoka ni mzoefu katika siasa za Tanzania na amewahi kushika nafasi mbalimbali zenye ushawishi.

Alikuwa Mbunge wa kuchaguliwa wa Jimbo la Same Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kati ya mwaka 2015 hadi 2020, ambapo alimshinda aliyekuwa Mbunge wa CCM, Anne Kilango Malecela.

Aidha, amehudumu kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa miaka 10 mfululizo, kuanzia mwaka 2015 hadi 2025.

Ujio wa Kaboyoka ndani ya ACT Wazalendo unaelezwa kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha nguvu ya chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025, hasa katika harakati za kujenga upinzani imara na chenye dira ya uwajibikaji wa kweli kwa wananchi.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...