Bondia Debora amtangazia vita Asia, apania kulipa kisasi

Na Winfrida Mtoi

Bondia  wa ngumi za kulipwa nchini, Debora Mwenda, ametangaza vita dhidi ya mpinzani wake Asia Meshack , akiahidi kulipa kisasi katika pambano la Dar Boxing Derby litakalofanyika Julai 26, 2025, jijini Dar es Salaam.

Amesema  pambano lililopita baada ya kupoteza alipata hasira kali hadi kulia ulingoni, hivyo bado ana machungu na hasira zote atazimaliza  mchezo ujao watakapokutana  tena na mpinzani wake.

“Nimuambie tu mpinzani wangu Asia kuwa bado nina hasira  ya mechi niliopoteza mbele yake na  nililia.  Namuambia ajipange maana hiyo hasira iliyonifanya ya nilie itakuja kumuishia yeye,” ametamba Debora.

Amesema mashabiki wake watarajie kuona mabadiliko ulingoni kwa kuwa amejipanga kuwapa burudani na kuondoka na ushini siku hiyo.

Hata hivyo amekiri kuwa mpinzani wake ni mzuri lakini amejiandaa vizuri kuhakikisha hawezi kurudia makosa yaliyomfanya apoteze pambano lililopita.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...