Dk. Mpango ashiriki Misa Takatifu iliyoongozwa na Papa Leo XIV, atembelea kampuni ya Health 3000

Na Mwandishi Wetu

Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango na mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wameungana na waumini mbalimbali wa Kanisa Katoliki Duniani kushiriki Dominika ya Ekaristi Takatifu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yohana wa Laterano lililopo Roma nchini Italia.

Misa hiyo imeongozwa na Papa Leo XIV. Makamu wa Rais yupo nchini Italia kumwakilisha Rais  Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na mikutano mbalimbali ya uwili.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais  ametembelea Kampuni ya Kimataifa ya Uzalishaji wa Vifaa Tiba ya Health 3000 jijini Roma, Italia.

Katika ziara hiyo, Dk. Mpango amefanya mazungumzo na viongozi wa kampuni hiyo, wakiongozwa na Mwenyekiti Maurizio Flammini na Mkurugenzi Mtendaji, Eleonora Flammini. Mazungumzo yao yakilenga kuimarisha ushirikiano katika sekta ya afya, hususani kwenye matibabu kwa njia ya mtandao (telemedicine).

Health 3000 ni mojawapo ya kampuni zilizo chini ya FG Group, inayojikita katika uzalishaji wa vifaa tiba kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Dk. Mpango yupo nchini Italia kumwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan), pamoja na mikutano mingine ya ‘uwili’.

spot_img

Latest articles

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...

Rostam aanika maono yake umiliki mpya ya NMG

Na Mwandishi Wetu MFANYABIASHARA na mwekezaji wa Tanzania, Rostam Azizi, ametangaza uwekezaji mkubwa wa kimkakati...

More like this

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...