Mwanamke ajiua kwa sumu  kisa mapenzi

Na Mwandishi Wetu

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Richard Abwao,  amesema mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Catherine Fito, mwenye umri wa miaka 21 mkazi wa Umanda Kata ya Kalunde Manispaa ya Tabora, amejiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu, huku chanzo cha kifo hicho ikiwa ni wivu wa mapenzi.

Akithibisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda  Abwao, amesema limetokea Juni 14,2025, ambapo mwanamke huyo anadaiwa kuwa katika mgogoro na mwenza wake kwa muda, hali iliyofanya kuchukua uamuzi huo.

“Tuna tukio moja la mwanamke kujiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu huko katika kijiji cha Umanda, Kata ya Kalunde Manispaa ya Tabora, aliyetambulika kwa jina la Catherine Fito mwenye umri wa miaka 21, ilipofika saa nne usiku siku ya tarehe 14 Mume wa marehemu alifika nyumbani kwake na kumkuta mwanamke huyo anagalagala chini nje  akiwa anatapika na alipumuuliza akajibu amekunywa sumu ya kuulia wadudu.

“Mgonjwa alipatiwa huduma ya kwanza katika zahanati ya Umanda na baada ya hapo akapewa Rufaa ya kwenda hospitali ya Milambo, lakini hawakufanya hivyo ndugu zake wakamchukua kumrudisha nyumbani na ilipofika saa kumi na mbili jioni siku ya tarehe 15 akafariki dunia akiwa nyumbani kwake na chanzo cha kifo hiki ni wivu wa kimapenzi.

spot_img

Latest articles

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...

KAIMU MSAJILI TPRB ASHIRIKI MAFUNZO ELEKEZI YA UONGOZI KWA WATENDAJI WAKUU WA TAASISI, MASHIRIKA YA UMMA NA WAKALA ZA SERIKALI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji (TPRB),...

More like this

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...