Wasira: Hatuahirishi Uchaguzi Mkuu ng’o

Na Mwandishi Wetu

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema hakitaahirisha uchaguzi ng’o kwa sababu kiliomba ridhaa ya kuongoza nchi kwa miaka mitano na kimeongoza vizuri kwa kuleta maendeleo chini ya serikali iliyoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Hayo yameelezwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira alipokuwa akiwasalimia wanachama, wapenzi wa Chama na wananchi waliofika ofisi za CCM Mkoa wa Ruvuma kumlaki akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo.

“Tuliomba ridhaa ya kuongoza Tanzania kwa miaka mitano, tumeiongoza Tanzania, tumefanya kazi yetu vizuri halafu unatuambia tuahirishe, ahirisha wewe mambo yako sisi hatuwezi ng’o, sisi tunagombea, tumeshaweka wagombea, tumemuweka Daktari Samia Suluhu Hassan (mgombea urais kupitia CCM), tumemuweka Dk. Emmanuel Nchimbi (Mgombea Mwenza wa CCM).

“Sasa wako rafiki zangu wale wa ‘tone tone’ wao wanapita wanawaambia tusifanye uchaguzi na mimi nawauliza tukiacha kufanya uchaguzi nchi itakuwa inaongozwa na nani, maana huwezi kuwaambia watu acheni uchaguzi halafu huwapi mbadala eti tuahirishe, tuahirishe nini?,” alieleza na kuhoji.

Alisema kuwa kote ambako wamepita na hata ambako bado hawajapita, CCM iko imara na inamuunga mkono Dk. Samia Suluhu Hassan na hawamuungi kwa sababu zozote ambazo hazielezeki, bali wanamuunga kwa sababu ya maendeleo makubwa aliyoyafanya “haya mnayoyasikia ameyafanya Songea ndiyo hayo hayo ameyafanya Tanzania nzima,”.

spot_img

Latest articles

Rais Samia asisitiza maadili kwa Jeshi la Polisi 

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan amewaasa wahitimu wa kozi ya maafisa na wakaguzi...

Rais Samia kupokea gawio la kihistoria, wachumi watarajia makubwa

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan,...

Dk. Mpango atoa wito  kwa Mataifa kupunguza uchafuzi wa mazingira, kulinda bioanuwai ya baharini

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango...

Serikali yatenga bilioni 43 kuimarisha michezo  shuleni

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imetenga  Sh 43 bilioni ili kuimarisha michezo katika...

More like this

Rais Samia asisitiza maadili kwa Jeshi la Polisi 

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan amewaasa wahitimu wa kozi ya maafisa na wakaguzi...

Rais Samia kupokea gawio la kihistoria, wachumi watarajia makubwa

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan,...

Dk. Mpango atoa wito  kwa Mataifa kupunguza uchafuzi wa mazingira, kulinda bioanuwai ya baharini

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango...