Rais Samia asisitiza maadili kwa Jeshi la Polisi 

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan amewaasa wahitimu wa kozi ya maafisa na wakaguzi wasaidizi wa Jeshi la Polisi kuwa mabalozi wa maadili na kusaidia kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea rushwa ndani ya Jeshi hilo.

Amesema hayo leo June 09,2025 Jijini Dar es Salaam wakati akishiriki sherehe ya kufunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi wa Jeshi la Polisi.

“Muwe sehemu ya kukomesha vitendo vya kuomba na kupokea rushwa. Haya ndiyo maradhi makubwa yaliyokuwa ndani ya Jeshi letu. Sitaki kusema yameisha, yapo, yanaendelea. Nikirushiwa clip (inayoonesha vitendo vya rushwa), namrushia IGP, na anachukua hatua mara moja,” amesema.

Rais Samia ameliagiza jeshi hilo kuhakikisha linaimarisha maadili kwa videndo kwa maafisa na askari wake ili melinda heshima ya taasisi hiyo na kuzidi kujenga imani ya wananchi kwa combo via dola.

Amesema  mafanikio ya  Jeshi la Polishi katika kulinda  raia na mali zao hayawezi kupatikana endapo maadili kudorora miongoni mwa watendaji wake.

Kuhusu usalama barabarani amelitaka jeshi hilo kuimarisha mikakati ya kuthibiti ajali za barabarani, akisema licha ya kushuka  kwa jumla ya idadi ya ajali na vifo katika mwaka  mmoja uliopita, bado takwimu za vifo ni kubwa.

Aidha amelitaka kuongeza ubunifu na matumizi ya teknolojia kabila kudhibiti ajali hizo.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...