Serikali yaja na mkakati kukabiliana na migogoro ya ardhi Morogoro

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Geophrey  Pinda amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na migogoro ya ardhi kati  ya wakulima na wafugaji katika maeneo mbalimbali hapa ikiwemo Mkoa wa Morogoro.


Ametoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma leo  Juni 6,  2025 wakati akijibu swali la Dk. Christine  Ishengoma Mbunge wa Vitu Maalum, aliyeuliuza ni upi mkakati wa Serikali wa kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji mkoani Morogoro?

Amesema hatua nyingine walizozichukua ni kupitia mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi (KKK) ambapo miji chipukizi kama ilivyo kwa miji ya halmashauri hupangwa, hupimwa na humilikishwa sambamba na kuweka mipango ya matumizi bora ya ardhi.

“Serikali inatambua kuwepo kwa migogoro ya wafugaji mkoani Morogoro, hata hivyo serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kukabiliana na migogoro hiyo ambapo baadhi ya hatua hizo ni  mipango ya matumizi bora za vijiji ili kubainisha maeneo ya kilimo sambamba na maeneo ya wafugaji kupitia Tume ya Matumizi Bora ya Ardhi,” amesema Pinda.

Aidha, Naibu Waziri Pinda ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha wanatumia ardhi kuendana na mipango ya matumizi iliyopangwa ili kuondoa muingiliano wa matumizi ya ardhi ambayo imekuwa chanzo cha migogoro ya wakulima na wafugaji.

spot_img

Latest articles

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...

KAIMU MSAJILI TPRB ASHIRIKI MAFUNZO ELEKEZI YA UONGOZI KWA WATENDAJI WAKUU WA TAASISI, MASHIRIKA YA UMMA NA WAKALA ZA SERIKALI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji (TPRB),...

More like this

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...